Mashirika ya umma lawamani Kiteto


Mashirika ya umma lawamani Kiteto

NA.MOHAMED HAMAD MANYARA
Mashirika ya umma wilayani kiteto mkoani Manyara yanayojihusisha na masuala ya matumizi bora ya ardhi pamoja na haki za binadamu yametupiwa lawama kwa kushindwa kuingilia kati migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji inayoendelea kurindima kila kukicha

Wakizungumza hayo wananchi wa mji wa Kibaya jana walisema hawaoni uwepo wa mshirika yanayojihusisha na matumizi bora ya ardhi na hata yale ya haki za binadamu kutokana na wakulima kuendelea kujeruhiwa na wafugaji kwa madai kuwa wanaharibu mazingira

Kwa sasa mashirika hayo ya umma yanayotajwa kuwa lawamani ni pamoja na shirika la KINNAPA,CORDS, NAADURARO na SWEAT, yanayofanya kazi wilayani kiteto ya matumizi bora ya ardhi

Mengine ni KIWOCOA,WASHEHABIKI, ambayo yanafanya kazi ya utetezi wa haki za binadamu kuwa kwa pamoja yameshindwa kuwa msaada katika sakata la wakulima na wafugaji wilayani hapo wanaohasimiana na hata kuuana

Kwakizungumxa juu ya sakata hili baadhi ya viongozi wa mashirika hayo kiwemo Joseph Kaaya wa shirika la WASHEHABIKI alisema kazi hiyo haina tija tena kwao baada ya kuundwa tume ya Waziri Mkuu Pinda kuchunguza mauaji hayoi

Mwisho

Maoni