Migogoro ya ardhi Kiteto itamalizwa na viongozi wa dini


Migogoro ya ardhi Kiteto itamalizwa na viongozi wa dini

NA.MOHAMED HAMAD MANYARA.
Serikali imeshauriwa kuacha kutumia Jeshi la Polisi kushuhulikia migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji Kiteto badala yake iwatumie viongozi wa dini ambao watatumia vitabu vitakatifu kurejesha amani inayoendelea kutoweka.

Kauli hiyo imetolewa na Mch.Richard Mwenda wa kanisa la Full Gospal Bible Felloship Kiteto mwishoni mwa wiki wakati akizungumzia njia ya kurejesha amani na athari wanazopata viongozi wa dini yanapojitokeza mauaji wilayani humo

“Hatuna amani viongozi wa dini tunapoitwa mara kwa mara kuzika watu wanaouawa tena kikatili kwa silaha za jadi,kuchinjana na hata kupigana risasi kutokana na migogoro ya ardhi mbona hapo mwanzo hatukuwa hivi?”alihoji Mch Mwenda

Alisema kazi ya viongozi wa dini ni kujenga watu kiimani ili wawe na hofu ya Mungu na mauaji ni matokeo ya watu kuwa na rogo ngumu iliyosababishwa na mfumo mbovu wa baadhi ya viongozi kuingia madarakani kwa kutumia ukabila

Kamati ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda iliyopo Kiteto inafanya kazi nzuri kuwarejesha watu katika misingi ya imani dhidi ya wenzao ambayo ilitoweka baada ya kugombanishwa na baadhi ya viongozi wasiowaadilifu kwa misingi ya kisiasa na ukabila

Kutumia Jeshi kukabiliana na wauaji ambao nao wanasilaha kamwe hawataweza kufanikiwa kamati ya Pinda iungwe mkoni na dini  na Serikali ifanikishe zoezi hilo na sio kutumia Jeshi la Polisi ambalo limesababisha madhara makubwa kwa wananchi

Awali Serikali ya Kiteto ilitumia Jeshi la Polisi katika kukabiliana na wakulima waliopo katika maeneo ya Emboley Murtangos kuwatoa kwa nguvu na hata kuteketeza mali zao kwa madai ya kuharibu mazingira

Kurejesha amani ni gharama na ni rahisi kuvunjika, Serikali ya Kiteto ilifanya kosa kutumika kama wakala wa jamii ya kifugaji wamasai kuwafukuza wakulima kwa gharama za wafugaji kuchanga mifugo yao jambo ambalo Waziri Mkuu alilikemea akidai ndicho chanzo cha migogoro hiyo

Akiwa katika mwendelezo wa mikutano na wananchi Mwenyekiti wa kamati ya maridhiano ya wakulima na wafugaji Askofu Amos Joseph Mhagachi alisema hatua iliyofikiewa inaleta matumanini ya kurejea amani Kiteto hasa wananchi wanapoendelea kutoa ushirikiano

“Tunaendelea kukutana na makundi mbalimbali ya wananchi wanatupa ushirikiano mzuri wa kuongea ukweli tena ukweli mtupu ambao hata sisi tunauona, sasa kamati hii sio mahakama tutaandika taarifa kisha kuiwasilisha kwa mwenyewe Waziri Mkuu”

Mwisho

Maoni