Mjamzito wa miezi 9 afariki kwa kugongwa na Bodaboda Kiteto


Mjamzito wa miezi 9 afariki kwa kugongwa na Bodaboda Kiteto

NA. Mohamed Hamad Manyara
Mwanamke mmoja mkazi wa eneo la Jangwani kata ya Bwagamoyo wilaya ya Kiteto mkoani Manyara amepoteza maisha baada ya kogongwa na pikipiki maarufu bodaboda wakati akitokea kliniki ya Hospitali ya Kiteto akielekea nyumbani kwake

Muda mfupi baada ya kufariki mwanamke huyo kwa zaidi ya saa moja mtoto amedaiwa kuendelea kucheza tumboni na baadaye alitulia wakati jitihada za kutaka kumpasua zikiendelea,  ndugu walikataa asifanyiwe upasuaji huo

Hata hivyo taarifa kutoka Hopitalini zinaeleza kuwa mwanamke huyo ambaye jina lake halikufahamika mapema alivunjika mguu na mkono huku dereva huyo naye akidaiwa kuwa hoi na amelazwa hospitali ya wilaya ya kiteto akijiuguza majeraha aliyoyapata baada ya kuburuzika

“Ndugu wa marehemu wamekataa asifanyiwe upasuaji baada ya vipimo kuwa mtoto naye amefariki hivyo wamemchukua kwaajili ya maziko ambayo yamefanyika saa saba mchana huu katika makaburi ya Jangwani”alisema mmoja wa watumishi wa Hospitali hiyo

“Ajali ilitokea jana saa tano za asubuhi muda mfupi baada ya mwanamke huyo kutoka kliniki na alipofika eneo la darajani njia ya kuelekea Handeni akagongwa na kijana aliyefahamika kwa jina la Kurwa Ramadhani (18) ambaye amelazwa hapa aliyekuwa akiendesha pikipiki maarufu bodaboda”kilisema chanzo cha habari

Kwakweli pikipiki zinakimbizwa sana barabarani na sio huyo tu aliyegongwa leo kuna mtoto mmoja wa Ibrahimu Elisha naye muda mfupi hapa kagongwa kavunjika mguu kaletwa hapa kwaajili ya matibabu kilizidi kueleza chanzo hicho

Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu huyo ambao hawakutaka kutajwa majina yao na ambao hawakutaka kuweka wazi juu ya suala hilo walisema wameamua kuuzika mwili huo ukiwa haujafanyiwa upasuaji wa kutoa kiumbe hicho cha miezi tisa tumboni ambacho nachi kimedaiwa kupoteza uhai

Baadhi ya wananchi waliozungumzia tukio hili akiwemo Ramadhani Issa alisema kilichofanywa na ndugu hao sio chakiungwana kwani walipaswa kukubali apasuliwe ili waone kama mtoto huyo yu hai ama amefariki na sio kuuzika mwili huo ukiwa hivyo

Jeshi la Polisi wilayani kiteto limekiri kutokea tukio hilo na kudai linaendelea kumshikilia kijana huyo aliyesababisha kifo cha mwanamke huyo na kwamba walidai chanzo cha ajali ni mwendokasi uliosababisha kushindwa kumudu pikipiki

mwisho


Maoni