MNEC Kiteto ahamasisha wananchi kusoma katiba


MNEC Kiteto ahamasisha wananchi kusoma katiba

NA.MOHAMED  HAMAD MANYARA
Mjumbe wa Halamshauri kuu ya CCM Taifa Emmanuel Papiani amewataka wananchi wilayani Kiteto mkoani Manyara kusoma kwa makini rasimu ya katiba pendekezwa kwa lengo la kuja kuipigia kura

Wilayani ya Kiteto imepata nakala 6900 ambazo zimegawanywa kwa makundi tofauti yakiwemo ya wananchi na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali kwa lengo la kusomwa

Akizungumza jana kwenye mfululizo wa mikutano aliyoanza vijijini mjumbe huyo alisema ameamriwa kuitish vikao hivyo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanasoma rasimu hiyo pamoja na kujiandaa kwa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura

“Rasimu pendekezwa ya katiba iligawanywa kata 19 zilizopo wilayani Kiteto na kwa taasisi za elimu, mashirika yasiyo ya kiserikali,taasisi za kidini na kwenye  maeneo ya mikusanyiko ya watu, someni muelewe kilichomo kisha mfanye maamuzi sahihi ya kuisaidia nchi”

Pia aliwataka wananchi hao kujiandaa kupokea daftari la kudumu la wapiga kura ambalo litaanza kwa wananchi kujiandikisha Mkoani Manyara baada ya mikoa mingine kumaliza

Baada ya kumalizika kwa hutuba hiyo wananchi wakapata fursa kutaka ufafanuzi wa kiongozi huyo juu ya mauaji yanayoendelea kujitokeza kuwa nini kauli ya chama baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu bila kusikia tamko lao

Awali akiuliza swali Neema Kivugo (mwananchi) kwa niaba ya akinamama alitaka kauli ya chama juu ya mauaji yanayoendelea hasa kwa wanawake na watoto kutokana na migogoro ya ardhi iliyodumu kwa miaka sita mfululizo

“Mhe Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa nini kauli yao juu ya kinachotokea Kiteto kwa akinamama na watoto wanaouawa kutokana na migogoro ya ardhi ambayo kwa sasa chama kimeendelea kuwa kimya”

Kwa upande wake Jastine Lukumay aliuliza lini chama kitachukua hatua ya kuzuia umwagikaji wa damu za watu wasio na hatia ili hali wanaoua wanafahamika huku Serikali ikiwa kimya?

Akijibu maswali hayo Mjumbe huyo wa Halamshauri Kuu ya CCM Taifa aliwataka wananchi hao kulaani mauaji hayo ambayo Taifa limesikia kilio chao na kuunda tume nyingi zilizofika kuchunguza na kuandika ripoti zao kisha kupeleka kwa uongozi wa ngazi ya juu

Christoph Parmet katibu mwenyezi wa CCM Taifa akitoa ufafanuzi kwa niaba ya chama alisema CCM haitasubiri wapinzani kuja kuwachambua juu ya kilichotokea bali wananchi wafanye maamuzi magumu ya kuwakataa viongozi wasiokuwa waadilifu

“Nilimshauri Mbunge wangu Benedict Ole Nangoro (CCM) katika vikao mbalimbali vya chama ajitokeze kwa wananchi kuonyesha hisia zake juu ya mauaji hayo akashindwa, kila mahali analalamikiwa naagiza marafiki zake waende kumwambi asipolaani mauaji hayo asije kusimama kwenye mikutano milele kupitia CCM kuomba kura”alisisitiza huku akipigiwa makofi mengi

Mwisho









Maoni