RC Manyara aunda tume kuchunguza migodi 16 iliyoungua.


RC Manyara aunda tume kuchunguza migodi 16 iliyoungua.

NA. MOHAMED HAMAD MANYARA
Mkuu wa mkoa wa Manyara Dr Joel Bendera ameunda tume ya kuchunguza chanzo cha moto uliotokea hivi karibuni katika migodi 16 ya Tanzanite kitalu B (Opec) iliyopo Mererani wilayani Simanjiro.

Moto uliunguza migodi ya wachimbaji wadogo  machi 8 saa 10 jioni na kusababisha hasara inayokadiriwa kuwa ya sh 2.4 bilion ambapo hata hivyo haukuleta madhata kwa watu kupoteza maisha

Akizungumza hayo mkuu huyo wa mkoa alisema wataalamu hao wamebobea katika Nyanja mbalimbali na kwamba watafanya kazi kwa uadilifu mkubwa ili kuweza kutoa majibu mazuri yatakayofanyiwa kazi na Serikali

“Nimeamua kuunda tume ili kuondoa manung’uniko ya wananchi juu ya kilichotokea kwani hakuna anayeonekana kusema jambo likakubalika bila kuleta utaalamu ambao utatusaidia Serikali na wananchi”alisema Bendera

Kwa upande wake Zacharia Lukas diwani wa kata ta Endiamtu alisema hatua hiyo itaondoa utata ambao umegubikwa baada ya kutokea tukio hilo ambalo wachimbani wadogo wameathirika

Hivi sasa baadhi ya wamiliki wa migodi hiyo wameathirika kwa kiasi kikubwa kwani moto uliteketeza kila kitu katika maeneo hayo ya migodi hiyo ambazo zilisaidia katika uchimbaji wa madini ya Tanzanite

Kwa upande wa wanachi waliozungumzia juu ya hatua hiyo walipongeza hatua hiyo wakisema ni mwafaka kwa sasa ambapo utata ulijitokeza juu ya chanzo cha moto huo ambao Tanesco waliruka kimanga kuwa hawakusababisha  wao

Mwisho

Maoni