Compassion wasaidia watoto 1243 Kiteto





Compassion wasaidia watoto 1243 Kiteto

NA. MOHAMED HAMAD MANYARA.
JUMLA ya wanafunzi 1243 ambao wazazi wao hawana uwezo wilayani Kiteto mkoani Manyara, wamepata ufadhili wa kusomeshwa na Compassion Interanation Tanzania kwa miaka 22 hapa nchini

Akizungumza siku ya mtoto wa Afrika mchungaji Dominick Chilambo wa kanisa la Anglikan KCC Kibaya alisema nafasi hiyo ni adimu kwa watoto hao ambao wengi wao wamekosa nafasi hizo kwa wazazi wao kutokuwa na uwezo wa kuwasomesha

“Najua nafasi hii ni adimu kuna watoto wenzenu wamebaki nyumbani hawaendi shule, ni kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo wazazi kushindwa kumudu gharama za masomo, na hata wengine kupata mimba nyinyi mmebahatika tumieni nafasi hii kupata elimu”alisema Mch.Chilambo

Alisema pamoja na wadau kujitokeza kuwasaidia mtoto kupata elimu kwa sasa wanakabiliana na changamoto nyingi zikiwemo mwamko mdogo wa wazazi kwa kuwatumia watoto wao kama vyanzo vya mapato kwa kuwaoza kwa wanaume

Alitaja sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo mzazi ana ridhaa kuozesha mwanae kwa mamlaka aliyonayo akisema, wengi wao wameolewa na wengine kupata ujauzito na kuacha shule kwa kukosa usimamizi makini wa wazazi na walezi wako

“Bado Serikali haijawa makini katika kuunda sheria ya motto, kwani mpaka sasa kuna sheria inasema motto ni yule mwenye umri wa chini ya miaka 18 lakini leo Taifa linashuhudia ndoa za utotoni watoto wa kike wakiozwa chini ya umri wa miaka 18”alisema

Kwa upande wake Joseph Kaaya mwangalizi wa haki za binadamu katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika alisema, kuwa imekosekana dhamira ya dhati kwa Serikali ya kumlinda mtoto ndidi ya maadui ambao hawapendi ajiendeleze kielimu

Hata sisi wanasheria tumekuwa hatuelewi cha kufanya kwani utamkamata mhalifu ambaye amesababisha mtoto kuacha shule na kumpeleka mahakamani lakini anakuja mzazi anasema nimemwozesha kwa ridhaa yake na sheria inamtambua alisema Kaaya

Nao wanafunzi katika risala yao mbele ya mgeni rasmi waliomba wadau mbalimbali wa elimu kuingilia kati kuhusu hujuma hizo kwa kushinikiza wabunge kubadilisha sheria kandamizi ikiwemo ya ndoa ambayo walisema kama hali hii haitakomeshwa miaka mitano ijayo watoto wa kike hawatakuwa na fursa kupata elimu

Jackson Abel Mkurugenzi wa kituo cha kanisa la TAG cha 127  akizungumzia fursa ya elimu inayotolewa na Compassion Internation Tanzania alisema kuwa mwanafunzi aliyyepokelewa ana nafasi ya kusomeshwa  kwa miaka 22 mfululizo na wafadhili pale ambapo atafuata masharti yao

Alitaja fursa kwa wanafunzi hao kuwa ni pamoja na kupatiwa mahitaji mbalimbali na wafadhili hao yakiwemo ada za shule,nguo,madaftari vitabu na hata kujengewa nyumba kwa wale wazazi wao wasiojiweza ili wajimudu kimaisha

Akifafanua zaidi Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika misaada hiyo kwa wanafunzi hao jumla ya Tsh 120 mil zimetumika kugharamia elimu na mahitaji ya shule kwa watoto hao

Zingine ni 10 mil zilitumika kwa masuala ya afya za watoto hao,20 mil zilitumika kuboresha makazi na hata kuwajengea nyumba baadhi ya watoto,na 30 mil zilitumika kugharimia mahitaji ya mtoto mmoja mmoja katika maeneo mbalimbali ya shuleni

Mwisho



Maoni