Ng’ombe 700 kutaifisha na Serikali Kiteto



Ng’ombe 700 kutaifisha na Serikali Kiteto

·       Wamiliki wadaiwa kuua na kujeruhi
·       Wananchi wapongea kamati ya ulinzi na usalama

NA.MOHAMED HAMAD
JUMLA ya ngombe 700  mbuzi na kondoo wapatao 290 wanakusudiwa kutaifishwa na Serikali wilayani Kiteto mkoani Manyara baada ya wamiliki wa mifugo hiyo kutokomea kusiko julikana kwa hofu ya kufunguliwa kesi ya mauaji yaliyomhusisha mkulima mmoja na kujeruhiwa wengine wane.

Mifugo hiyo iko chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi imehifadhiwa uwanja wa mpira wa miguu Kiteto kwa siku tatu mfululizo kusubiri wenyewe kujitokeza bila mafanikio na kwamba jitihada za kuinusuri ni kuitaifisha na kuipeleka ranchi ya Taifa ili iweze kuhudumiwa

Waliolazwa ni pamoja na Dominic Meena (48) ,Daudi Eraston (22) Selemani Chizenga (33) na mmoja ambaye jinalake halijafahamika kwa pamoja walipata majeraha vichwani  pamoja na kuvunjwa mikoni na vidole

“Tatizo linalojitokeza hapa kuna baadhi ya viongozi ambao wanashindwa kutambua nafasi zao ndani ya jamii, ona hapa kuna madiwani wanaotokana na jamii ya kifugaji wanafika eneo la tukio na huenda wanaifahamu mifugo hiyo lakini wanashindwa kutoa ushirikiano pamoja mifugo hiyo kuwa na alama za wamiliki”

“Kwa sasa kama hawatajitokeza mpaka kesho tutashauriana kuona namna ya kuokoa mifugo hiyo kwa kuitaifisha na kuipeleka ranchi ya Taifa ili ziweze kuendelea kuhudumiwa na Serikali mpaka hapo mmiliki atakapo jitokeza”alisema George Katabazi OCD Kiteto

Baadhi ya madiwani waliofika kushuhudia mifugo hiyo uwanjani ni pamoja na Sekemi Sakana diwani wa kata ya Partimbo ambako mauaji yamefanyika na Yohana Bakar diwani kata ya Namelock ambazo ni kata za jamii ya kifugaji (maasai)

Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Kiteto Kanali Samuel Nzoka aliambia Jambo Leo kuwa kitendo cha jamii ya kifugaji wamasai kususia Serikali mifugo yao ni kosa ambalo halivumiliki na sio utetezi kwa wakosaji na kuwataka wajitokeze ili kuchukua mifugo yao na sheria ifuate mkondo wake

Alisema mifugo hiyo inahitaji kuhudumiwa kwa kupelekwa malishoni na hata maji hivyo toka ikamatwe haijapata huduma hizo na kwamba madhara yanaweza kujitokeza kama itaendelea kubaki katika eneo hilo yakiwemo vifo

Kwa upande wake Bakari Maunganya mwenyekiti wa wakulima  wilayani Kiteto amelaani mauaji hayo na kuishukuru kamati ya ulinzi na usalama kuwa imekuwa msaada mkubwa katika kukabiliana na uhalifu huo

Alisema kila mara wafugaji wameendelea kutenda uhalifu kwa kuwaonea wakulima wanapokuwa shambani kupigwa na hata kuuawa lakini hawajawahi kutiwa hatiani kwa tuhuma hizo huku mauaji yakiendelea

“Kwa sasa watu 41 wamepoteza maisha kutokana kuvamiwa wakiwa shambani na jamii ya wafugaji wamasai huku uongozi wa Wilaya ukikiri jamii hiyo kuwa tishio kwa kufanya uhalifu mara kwa mara”alisema Maunganya

Kwa mujibu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Manyara Kamishna msaidizi Christopher Fuime amekiri kutokea tukio hilo na kudai kuwa jumla ya watu wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi na mara uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani

Mwisho

Maoni