Afisa maendeleo ya jamii ajitosa Ubunge Kiteto.




Afisa maendeleo ya jamii ajitosa Ubunge Kiteto.

NA. MOHAMED HAMAD.
Afisa maendeleo ya jamii wilaya ya Kiteto mkoani manyara Joseph Mwaleba, amejitosa kugombea Jimbo la Kiteto kupitia chama cha Mapinduzi CCM lililokuwa linaongozwa na Benedict Ole Nangoro

Nitahakikisha naduisha amani iliyokwisha kutoweka kwa miaka zaidi ya saba huku viongozi wakishindwa kuunganisha jamii ya wafugaji na wakulima ambao kila mara huuana

Akieleza hayo kwenye viwanja vya CCM wilayani humo mwishoni mwa wiki aliporejesha fomu hiyo Mwaleba alisema Kiteto ina matatizo makubwa ambayo hadi sasa hakuna kiongozi aliyefanikiwa kuyatatua

“Kwa muda mwingi niliokaa hapa Kiteto kama mtumishi wa Serikali,Afisa Maendeleo ya Wilaya sijaona kilichofanyika kuhusu amani ya Kiteto na badala yake kila kukicha wananchi wameendelea kufa wakigombea ardhi”alisema Mwaleba

Katika maelezo yake hayo Mwaleba alisema njia atakayotumia kukabiliana na tatizo hilo ni kuwakutanisha wakulima na wafugaji ili waweze kuzungumza matatizo yao hayo na kuridhiana

Alitaja kipao mbele chake kingine ni kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja ili kuondokana na umaskini uliokithiri kwa miaka mingi kwa kutumia elimu ya ujasiria mali

Mbali na ofisa huyo wengine waliochukua fomu ni Hajjat Amina Said Mrisho,Benedict Ole Nangoro anaye tetea Jimbo hilo,Emmanuel Papian na Ally Juma Lugendo

Baadhi ya wananchi waliozungumza na Jambo leo walielezea kuwa Jimbo la Kiteto linahitaji mtu makini, mwenye nguvu ya ushawishi, anayekubalika kwa jamii zote za wakulima na wafugaji

Kwa kipindi chote hicho wananchi hao wameshindwa kufanya shuhuli za maendeleo na kuishi kwa wasiwasi kuhofia kuuawa huku umaskini ukizidi kushika hatamu na kushindwa kuchangia maendeleo yao

MWISHO



Maoni