BVR Kiteto yafanikiwa kwa 75.3%




Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto Bosco Ndunguru akifafanua jambo kuhusu BVR Kiteto kushoto ni Mainge Lemalali mwenyekiti wa Halmashauri.

BVR Kiteto yafanikiwa kwa 75.3%

NA.MOHAMED HAMAD
ZOEZI la uandikishaji wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa njia ya BVR awamu ya kwanza kati ya awamu nne wilayani Kiteto mkoani Manyara limefanikiwa kwa 75.3%.

Awamu ya kwanza imehusisha kata za mashariki mwa wilaya ya Kiteto ambako ni kata za Kijungu,Loolera,Lengatei na Sunya ambapo jumla ya watu 17743 wameandikishwa

“Akizungumza na Jambo leo Bosco Ndunguru afisa mwandikishaji wa wilaya na Mkurugenzi Mtendaji alisema zoezi hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika maeneo hayo tofauti na ilivyotegemewa”

Alisema zoezi lilianza juni 16 mwaka huu, kata ya Kijungu imeandikisha watu 2907 sawa na 87.27% kati ya 3331,huku Lengatei ikiandikisha watu 4718 sawa na 80% kati ya watu 5842 waliokusudiwa kuandikishwa

Kata ya Loolera jumla ya watu 2235 sawa na 77.3% wameandikishwa  kati ya watu 2889 waliokusudiwa kuandikishwa huku kata ya Sunya ikifanikiwa kuandikisha watu 7883 sawa na 68.64% kati ya 11483 waliokusudiwa kuandikishwa

Kwa mujibu wa Ofisa mwandikishaji wa wilaya alitaja changamoto zinazokabili zoezi hilo kuwa ni pamoja na watu kutojitokeza kwa wingi akisema jitihada zinafanyika kwa kutumia gari la matangazo kuhamasisha watu kujiandikisha

Kuhusu mashine za BVR alisema jumla ya mashine tano ziiliharibika na kwamba zinaendelea kushuhulikiwa na mafundi huku zingine zikitarajiwa kuingia kwaajili ya zoezi hilo

“Kuna mashine tano zinafanyiwa marekebisho baada ya kusumbua, wapo mafundi wanaoendelea nazo niwaahidi tu wananchi kuwa wote wataandikishwa katika daftari hili la kudumu”alisema Ndunguru

Kwa upande wake Ally Mzigo mwenyekiti wa Kijiji cha Sunya (CHADEMA) alisema kituo  cha Fachande kilichopo ofisi ya Kijiji kimesimama kuandikisha na hakuna maelezo yoyote kutoka kwa waandikishaji

Kwa mujibu wa Ofisa uandikishaji wa wilaya alikiri na kudai kuwa tatizo hilo akidai limetokana na  kukosekana kwa wino ambao umeagizwa mkoani Manyara na mara baada ya kufika zoezi litaendelea

Kwa upande wa wananchi waliozungumzia zoezi hilo wamedai tatizo lililopo ni kukaa muda mrefu vituoni hali inayofanya wakate tamaa na kurejea nyumbani kwaajili ya kutafuta riziki

MWISHO




NA.MOHAMED HAMAD
ZOEZI la uandikishaji wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa njia ya BVR awamu ya kwanza kati ya awamu nne wilayani Kiteto mkoani Manyara limefanikiwa kwa 75.3%.

Awamu ya kwanza imehusisha kata za mashariki mwa wilaya ya Kiteto ambako ni kata za Kijungu,Loolera,Lengatei na Sunya ambapo jumla ya watu 17743 wameandikishwa

“Akizungumza na Jambo leo Bosco Ndunguru afisa mwandikishaji wa wilaya na Mkurugenzi Mtendaji alisema zoezi hilo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika maeneo hayo tofauti na ilivyotegemewa”

Alisema zoezi lilianza juni 16 mwaka huu, kata ya Kijungu imeandikisha watu 2907 sawa na 87.27% kati ya 3331,huku Lengatei ikiandikisha watu 4718 sawa na 80% kati ya watu 5842 waliokusudiwa kuandikishwa

Kata ya Loolera jumla ya watu 2235 sawa na 77.3% wameandikishwa  kati ya watu 2889 waliokusudiwa kuandikishwa huku kata ya Sunya ikifanikiwa kuandikisha watu 7883 sawa na 68.64% kati ya 11483 waliokusudiwa kuandikishwa

Kwa mujibu wa Ofisa mwandikishaji wa wilaya alitaja changamoto zinazokabili zoezi hilo kuwa ni pamoja na watu kutojitokeza kwa wingi akisema jitihada zinafanyika kwa kutumia gari la matangazo kuhamasisha watu kujiandikisha

Kuhusu mashine za BVR alisema jumla ya mashine tano ziiliharibika na kwamba zinaendelea kushuhulikiwa na mafundi huku zingine zikitarajiwa kuingia kwaajili ya zoezi hilo

“Kuna mashine tano zinafanyiwa marekebisho baada ya kusumbua, wapo mafundi wanaoendelea nazo niwaahidi tu wananchi kuwa wote wataandikishwa katika daftari hili la kudumu”alisema Ndunguru

Kwa upande wake Ally Mzigo mwenyekiti wa Kijiji cha Sunya (CHADEMA) alisema kituo  cha Fachande kilichopo ofisi ya Kijiji kimesimama kuandikisha na hakuna maelezo yoyote kutoka kwa waandikishaji

Kwa mujibu wa Ofisa uandikishaji wa wilaya alikiri na kudai kuwa tatizo hilo akidai limetokana na  kukosekana kwa wino ambao umeagizwa mkoani Manyara na mara baada ya kufika zoezi litaendelea

Kwa upande wa wananchi waliozungumzia zoezi hilo wamedai tatizo lililopo ni kukaa muda mrefu vituoni hali inayofanya wakate tamaa na kurejea nyumbani kwaajili ya kutafuta riziki

MWISHO

Maoni