SAKATA LA UCHAGUZI KITETO.Katibu CCM Kiteto afungiwa ndani ya Ofisi.








SAKATA LA UCHAGUZI KITETO.

Katibu CCM Kiteto afungiwa ndani ya Ofisi.
·                    Wamasai walinda mlango kwa silaha za jadi
·     
                  Aokolewa na Polisi,10 wakamatwa
NA.MOHAMED HAMAD MANYARA.
KATIBU wa chama cha mapinduzi CCM Wilayani Kiteto mkoani Manyara Abeid Maila, amejikuta katika wakati mgumu baada ya vijana wa jamii ya kifugaji (morani) masai, kuvamia ofisi ya chama na kufunga mlango huku wakilinda kwa silaha za jadi.

Tukio hilo limetokea julay 31 mwaka 2015 saa 4:30 asubuhi baada ya katibu huyo wa CCM Wilaya kukataa kupokea majina ya wanachama zaidi ya 8000  kata ya Namelock na Sunya yalidaiwa kucheleweshwa

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa katibu huyo zilisema, mwisho wa kuwasilisha majina ya wanachama kwaajili ya maandalizi ya uchaguzi ulikuwa tarehe 15.7.2015 ambapo vijana hao waliyaleta tarehe 31.7.2015 siku moja kabla ya uchaguzi

“Hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea, hawa vijana niliwaelekeza toka mwanzo kuwa mwisho wa kuleta majina ya wapiga kura ni julay 15 na hata wagombea wao wanajua walikwisha kutaarifiwa sasa kitendo cha kulazimisha ni ishara tosha kuwa wanamsukumo kutoka kwa wagombea wao”alisema Katibu huyo

Alisema majina ya wanachama wote wa CCM yamewasilishwa mkoani, na idadi inafahamika hivyo kutenda cha vijana hao kuja na majina hayo ni ishara tosha kuwa wanaanza kuleta vurugu kutaka kuharibu uchaguzi mzima wa kura za maoni

Wakati sakata hilo likijitokeza kamati ya Siasa ya Wilaya ilikuwa inaendelea na vikao vyao kwaajili ya maandalizi ya uchaguzi wa kura za maoni kesho (leo) kwamba kupokelewa kwa wanachama hao kutampa nafuu mmoja wa wagombea ubunge kati yao

Taarifa za uhakika kutoka katika vyanzo mbalimbali vya habari hizi zinasema kuwa, utaratibu huu ndio unaotumika kila mara wilayani humo kujihakikishia ushindi kwa mgombea ambapo ilielezwa kuwa idadi hiyo ya kura ni nyingi na haijapata kutokea

Kwa Mujibu wa Joseph Mwaleba mmoja wa wagombea ubunge (CCM) katika maelezo yake na gazeti hili alisema sakata hili liliibuka siku tatu zilizopita wakimzuia mbunge anayemaliza muda wake Benedict  Ole Nangoro kulazimisha majina hayo kupokelewa

“Tumekuwa tukigombana sana na huyu mwezetu kulazimisha vitu nje na sheria, mfano tuliambiwa mwisho wa kuleta majiana hayo ni tar 15 mwezi huu lakini alizidi kulazimisha akitaka kiasi hicho kipokelewe jambo ambalo ni kinyume na utaratibu”alisisitiza Mhombea huyo

Naye Emmanue Papian Mgombea wa (CCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa alisema mbali na vioja hivyo, kumekuwepo na ubaguzi wa ukabila uliokuwa unaendelea na kwamba amezitaka mamlaka husika kuingilia kati na kuona haki ikitendeka kwa maslahi ya Taifa

“Naviamini  vyombo vya usalama vya chama na Taifa vitatenda haki, kwani kwa miaka zaidi ya 50 sasa hatuwezi kuendelea kuuzungumzia ukabila na hata ubaguzi wa rangi ni dhambi kubwa na mbaya”alisisitiza Papian

Kukamatwa kwa wanachama hao wa CCM na kufikishwa Polisi kumewagawa wajumbea wa Halamshjauri kuu ya CCM Wilaya kwa msingi wa ukabila ambapo miongoni mwao walisikika wakisema tutaenda kuwatoa kwa gharama zozote

“Naamini hilo sio kosa la kutisha, watatoka tu ngoja tumalize kikao hapa, kwani walichokifanya kiko katika kosa gani la kisheria” alizidi kulalata mjumbe huyo wa kamati ya Siasa ya CCM Wilaya na kuingia ndani baada ya mlango kufunguliwa

Katibu huyo wa CCM Wilaya ameripoti polisi kwaajili ya mahojiano zaidi, kwamba mara baada ya kumaliza anatakiwa kuhakikisha kuwa kesho (leo) uchaguzi unafanyika na wanachama wa CCM wanapata wawakilishi watatu watakaoenda kuchunjwa mkoani

Kwa upande wa baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo walisema kuwa hiyo ni ishara tosha kuwa mwaka huu kutakuwa na mabadiliko makubwa ya utawala, kwani toka Wilaya izinduliwe mwaka 1974 hayajapata kutokea

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kiteto zaidi ya vijana 10 wa jamii ya kifugaji wanashikiliwa kwaajili  ya mahojiano zaidi juu ya tukio hilo  na mara baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zitakazowakabili

Mwisho

Maoni