Wagombea Ubunge CCM Kiteto waingia mitini.

Wagombea Ubunge CCM Kiteto waingia mitini.
·                                  
                  Wahofu kuwafanyia fujo,wananchi wawashangaa

NA.MOHAMED HAMAD KITETO.
MKUTANO wa kuwanadi makada watano wa chama cha mapinduzi CCM nafasi ya Ubunge kata ya Kibaya Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, umeingia dosari baada ya wagombea hao kuingia mitini wakihofia kurushiwa mawe na kuzomewa.
                                   
Awali wagombea hao walifanya mkutano wa kampeni katika kata za Bwagamoyo na Kaloleni wilayani humo, huku wananchi wakihoji hatma ya maisha yao kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji iliyodumu kwa muda mrefu

Katika mikutano yote iliyofanyika ya kampeni, wananchi hawakusita kuhoji juu ya migogoro hiyo, huku wakipatiwa majibu na mbunge anayemaliza muda wake ambapo walidai kutoridhika wakisema wapatiwa majibu sahihi

“Haiwezekana hata kidogo kuambiwa eti mbunge wetu hakuhudhuria mazishi na hata kutoa pole kwa wahanga wa migogoro ya ardhi akidai alikuwa na kazi maalumu…mbona tunashuhudia maeneo mengine wabunge wao wanakemea vitu kama hivi katika majibo yao?alihoji mmoja wa wananchi hao

Akizungumza hayo Bakari Maungaya (mwananchi) alisema kitendo cha wagombea hao kuingia mitini na kukimbilia vijijini kujinadi inatosha kuwa hawawatendei haki wananchi hasa wale wanaojitambua mijini na badala yake wanakimbilia vijijini

“Kama kweli wagombea wanatambua wajibu wao sehemu ya kujipima ilikuwa maeneo ya mijini sasa kama watawakimbia wananchi wa mijini hawaoni kuwa huko ni kufilisika kisiasa”alisema huku akionyesha kuchukizwa na tabia hiyo

Hata hivyo Suleyman Kaberwa mwenyekiti wa CCM kata ya Kibaya akizungumza na umati wa wanachama hao wa CCM alisema amekerwa na kitendo hicho akisema wengi wa wagombea hao hawakuwa tayari kufika kwenye eneo hilo la kampeni

“Huko jamani tumegombana sana kuwakutaka kuja lakini wengi walikataa wakisema wanahofia maisha yao,baada ya kuona vijana wetu wa bodaboda kupamba msafara wa wagombea wakati wakitokea kata za jirani”alisema

Kwani kupambwa kwa msafara kwa mfumo wa kuwa na pikipiki hili ni geni kwenu jamami?.....hapanaaa sasa tatizo nini hili limeniuma sana najua nimetimiza wajibu wangu japo kuja kuwaambua kilichotokea alimalizia Kaberwa

Kwa upande wake Emmanuel Papian akizungumza na Jambo leo kuhusu tuhuma za wagombea kuingia mitini alisema amekerwa na wenzake ambao mara zote aliwataka waende kwenye mkutano baada ya kutoka kata za jirani na kukataliwa

“Niliwasihi sana wenzangu nikawaambia twendeni wananchi wanatusibiri lakiki walionekana kuwa wazito huku wakisema usalama wao ni mdogo jambo ambalo, niliwaambia kuwa hiyo ni kazi ya Polisi kutulinda kama kuna shida lakini walikataa

Kwa upande wa katibu wa CCM Wilaya Abeid Maila alisema ilikuwa vigumu kuwalazimisha wagombea kuingia kwenye kikao huku wakikataa kwenda hivyo alichofanya ni kuahirisha kwa kuwataka wajhiandae kumalizia kata ya Kijungu na Loolera

Mwisho



Maoni