CELG wakabidhi vitendea kazi,wasaidizi wa kisheria





CELG wakabidhi vitendea kazi,wasaidizi wa kisheria

Na.Mohamed Hamad Kiteto
KITUO cha sheria za mazingira na utawala (Center for Enviromental Law and Governance) chenye makao  yake makuu Dar es Salaam, kimetoa msaada wa vifaa vya ofisi kwa wasaidizi wa kisheria 25 wilayani Kiteto, kwaajili ya kuwawezesha kuweka kumbukumbu

Vifaa hivyo ni mafaili ya Ofisi,Scanna moja pamoja na machapisho mbalimbali ambayo yatasaidia katika kazi ya usaidizi wa kisheria wilayani Kiteto juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaoendelea kujitokeza wilayani humo

Akikabidhi vifaa hivyo kwa mratibu wa wasaidizi wa kisheria wilayani Kiteto mwanasheria wa kituo hicho Elizabeth Maganga  alisema vifaa hivyo vitumike kuhifadhia taarifa za kituo hicho zinazokusanywa kutoka kwa wateja wao

“Naamini sasa taarifa zenu zitakuwa na usiri wa hali ya juu kwani mtakuwa mmezihifadhi kwenye mafaili, na pia mtatuma taarifa kwetu kwa urahisi kupitia mitandao ambapo mtaziskan na kuzituma kiurahisi ”alisema mwanasheria huyo

Awali taarifa hizo zilionekana kutokuwa na usiri wa kutosha pamoja na changamoto za kutuma taarifa hizo makao makuu jambo ambalo lilikuwa na changamoto kubwa kwa wasaidizi hao wa kisheria Wilayani humo katika utendaji wao wa kazi

Akishukuru baada ya kukabidhiwa msaada huo Mwadawa Ally mratibu wa wasaidizi wa kisheria Wilayani Kiteto alishukuru kituo hicho cha CELG akisema, msaada huo umefika wakati mwafaka ambao kila mmoja atawajibika katika nafasi yake ipasavyo

“Tulihitaji kufanya kazi ya usaidizi wa kisheria kwa kiwango cha hali ya juu, sambamba na kuhifadhi vizuri kumbukumbu zetu sambamba na kuzituma kwa wakati, naamini kazi hiyo itafanyika kwa umakini wa hali ya juu”alisema Mwadawa

Mbali na msaada huo washiriki hao wanaendelea na mafunzo ya siku tano kuhusu aina za ukatili wa kijinsi na sheria zake pamoja na kuunda mikakati ya kuzuia ukatili wa kijinsia unaoendelea kujitokeza kila kukicha wilayani humo

Mwisho

Maoni