CHADEMA Kiteto wampiga “stop”mwenyekiti kushiriki kampeni





 Mbunge viti maalumu CHADEMA Paulina Gekuli akiongea na wajumbe wa BAWACHA Kiteto hivi karibuni, kulia mwenye koti jeusi ni mwenyekiti wa wilaya ya Kiteto CHADEMA tabrani Msangi aliyesimamishwa nafasi hiyo kwa madai ya kumnadi mgombea wa CUF kuwa Mbunge Jimbo la Kiteto

CHADEMA Kiteto wampiga “stop”mwenyekiti kushiriki kampeni

NA. Mohamed Hamad Manyara
CHAMA cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoani Manyara, kimemsimamisha kazi mwenyekiti wa wilaya ya Kiteto Tabrani Msangi, kushiriki kampeni za uchaguzi zinazoendelea kutokana na madai kuwa amekisaliti chama na kumnadi mgombea wa CUF kwa nafasi ya Ubunge

Hayo yalielezwa kwenye uzinduzi wa kampeni za chama hicho kata ya Matui siku moja baada ya mwenyekiti wa huyo wa wilaya Tabran Msangi kumnadi Hassani Losioki mgombea wa CUF katika mkutano ulioitwa kuwa ni wa uzinduzi wa Ukawa mjini Kibaya

“Kuanzia leo Tabran Msangi ni marufuku kushiriki kampeni za CHADEMA zinazoendelea sasa kama mwenyekiti kutokana na kitendo cha kukihujumu chama kwa kumnadi Hassan Losioki akidai kuwa ni mgombea aliyetokana na Ukawa”alisema katibu wa CHADEMA mkoa wa Manyara

Alisema mwenyekiti huyo toka awali alionekana kuwa msaliti, na chama kilikuwa kinafuatilia nyendo zake na ndio maana katika hali isiyotazamiwa alijitokeza hadharani kwenye mkutano wa CUF na kumnadi mgombea wao

Katika kikao alichoshiriki mwenyekiti Tabrani kumnadi mgombea wa CUF alisema CHADEMA imefanya mabadiliko ya kumteua mgombea mwingine ambaye ni Hassan Losiok kuwa ndiye atakayepambania jimbo la Kiteto kuwa Mbunge

Alisema mgombea Ubunge Kidawa Othman wa CHADEMA hana sifa, ana elimu ya darasa la nne hivyo hawezi kuingia Bungeni kwa elimu hiyo na nafasi anayoiomba ya Ubunge ni kazi kubwa ambayo kwa sasa haiwezi

Akiomba ridhaa kwa wananchi Kidawa Othman alisema, anatosha katika nafasi hiyo na kitendo cha kuaminiwa na chama chake ni ishara tosha kuwa anauwezo wa kuwatumikia wananchi katika kujiletea maendeleo ya pamoja

“Siwezi kuwa mzigo Bungeni,tumekuwa tukikosea sana kuchagua watu wenye sura ya ukabila,uchoyo na ufisadi katika nafasi ya Ubunge ambao wamekuwa tatizo ambalo limesababishia wananchi madhara yakiwemo ya maafa”alisema

“Tazama tumekuwa katika mgogoro mkubwa kati ya wakulima na wafugaji, hii ilisababishwa na viongozi wetu waliolewa madaraka na kujiingiza katika manufaa yaliyoleta madhara yakiwemo yale ya watu zaidi ya 40 kuuawa na wengine kujeruhiwa”

Alisema kuwa atakapochaguliwa kuwa mbunge atahakikisha kuwa anaondoa ukabila uliochimbiwa mizizi kwa watu kuchukiana kati ya wakulima na wafugaji ambapo ilisababisha serikali kutumia fedha nyingi kuja Kiteto kufanya uchunguzi juu ya mauaji hayo

mwisho

Maoni