Dunni akacha mkutano Kiteto



Dunni akacha mkutano Kiteto

Mohamed Hamad

Kiteto.Mgombea mwenza wa Urais kupitia vyama vinne vilivyoungana kupitia katiba ya wananchi Ukawa Dunni Hajji Dunni, ameukacha mkutano ulioandaliwa na CUF wilayani Kiteto kutokana na  mvutano wa kisiasa kati ya CHADEMA na CUF

Mvutano huo ulimsababisha Mgombea Urais kupitia Ukawa Endward Lowassa kushindwa kumnadi mgombea wa Jimbo la Kiteto kutokana na sakata hilo hivi karibuni ambao kwa sasa siasa za Kiteto zimedaiwa kuchukuwa sura mpya kwa wananchi

Akiwa mjini Kibaya akitokea wilaya ya Chemba Dunni aliandaliwa mkutano chini ya viongozi wa CUF wilaya ambapo walitangazia kuwa watapata fursa ya kumsikiliza mgombea huyo sambamba na kumnadi mgombea wao wa Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CUF

“Taarifa zilisema kuwa Dunni hajji atazungumza na wananchi saa 3-4 asubuhi, tulishuhudia wananchi wakiendelea kusogea kwenye mkutano na baadaye Dunni alitokea katika maeneo ya mkutano bila kushuka na kuaga baadhi ya viongozi akiwemo Kidawa wa CHADEMA ”alisema mmoja wa viongozi wa wilaya hiyo

Ujue huu mkutano haukuwa kwenye ratiba tulishangaa wenzetu wa CUF wakiuandaa kwa nguvu zote na ndio waliowatangazia wananchi kuwa utafanyika, sasa wananchi wameonekana kuchukizwa sana na kitendo hicho wakati wakiondoka kwenye mkutano huo,alisema Tikima Rashidi mwenyekiti wa CUF wilaya ya Kiteto

“Tulitegemea Dunni amtangaze Hassani Losioki kupitia CUF mgombea ubunge Jimbo la Kiteto ndio anayeungwa mkono na wananchi, kitendo cha kuondoka ikizingatiwa Lowassa alifika na kuahidi kuwa hatma ya Kiteto itatokana na maamuzi ya chama makao makuu kuondoka kwake ametuacha njia panda”alisema Tikima

Mgogoro wa kisiasa kwa wagombea ubunge wa Jimbo la Kiteto kati ya CHADEMA na CUF unazidi kuchukua sura mpya baada ya wagombea hao kuzidi kutunishiana mizuli majukwaani kwa kutuhumiana kuwa ni pandikizi la CCM

Kidawa Othmani anayegombea kupitia CHADEMA katika mikutano yake alisema kuwa yeye ndiye aliyeteuliwa na vyama vilivyoungana Ukawa kugombea Jimbo la Kiteto, huku Hassani Losiok naye katika mikutano yake akiwaambia wananchi kuwa ndiye mgombea pekee

Wakati hayo yakijitokeza wanachama wa vyama vya upinzani wilayani humo wamedaiwa kuwa njia panda kuona wagombea hao wakiendelea kusuguana huku zikiwa zimebaki siku chache kuingia kwenye uchaguzi mkuu ambao watatakiwa kufanya maamuzi

Wadadisi wa masuala ya kisiasa wakizungumza na gazeti hili walisema mgawanyiko huo ni furaha kwa CCM ambapo watagawana kura na kumfanya ashinde kwa kura nyingi

“Ujue mvutano huu umetokana na baadhi ya wagombea ubunge walioangushwa kupitia CCM wafuasi wao kuhamia vyama vya upinzani na kufanya wananchi washindwe kuwa sasa nani anafaa na kwa sababu gain,ikumbukwe hata elimu ya uraia haikutolewa”alisema Bakari Maunganya mwananchi

Mwisho

AHSANTE KWA KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZETU PIA KUJITANGAZA NASI IWAPO UNAHABARI AMA TANGAZO WASILIANA NASI 0758 222 248/0787 055080
Email . masarade1995@gmail.com ,
ANGALIZO KUMBUKA KILA MMOJA ANA MTAZAMO WAKE HIVYO TUMIA LUGHA NZURI KATIKA KUTOA MAONI YAKO IWAPO UTASHINDWA BASI NI HERI USITOE MAONI SI LAZIMA ILI KUEPUSHA MAKWAZO KWA MWINGINE

Maoni