Malaigwanani Kiteto waridhia mpango wa uzazi






Malaigwanani Kiteto waridhia mpango wa uzazi

Na. Mohamed Hamad
Zaidi ya viongozi wa mila mia moja wa jamii ya kifugaji maasai pamoja baadhi ya viongozi wa Serikali za vijiji wilayani Kiteto mkoani Manyara, wameazimia kujiunga na mpango uzazi salama

Wakizungumza kwenye kongamano lililoandaliwa na Halmashauri ya wilaya kwa ushirikiano na Engenda Helth viongozi hao wa mila walisema ongezeko la vifo vya wazazi,watoto wachanga na watoto chini ya miaka mitano linazidi kuwa tishio

“Hatuwezi kuendelea kushuhudia vifo vya mama na mtoto na kila mara kwa kuendeleza mila na tamaduni za makabila yetu,kwani madhara tunayaona kazi tutakuwa nayo sasa ni kuhakikisha elimu hii inawafikia wananchi wetu”alisema Mbambire Oleikurukuru

Alisema kongamano hilo ni matokeo ya kikao maalumu kilicho fanyika kuwataka viongozi hao ambao wanaushawishi mkubwa ndani ya jamii kuhamasisha jamii kutumia mpango wa uzazi salama na kuzuia maambukizi ya VVU Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa motto

Pia mafunzo hayo yalihitaji wanaume kushiriki huduma za afya ya uzazi,huduma za uzazi wa mpango na uchaguzi wa saratani ya shingo ya kizazi na mama kuwa salama anapojiandaa kubeba ujauzito hadi arobaini ya uzazi

Wakati wa ujauzito mama anatakiwa kuwahi kliniki kabla ya wiki 12 ili aweze kupata huduma zote kama vile upimaji wa VVU Ukimwi na magonjwa kama vile kaswende,kupima kiasi cha damu,kupewa dawa za kinga ya malaria na za madini chuma na dawa ya minyoo

Mbali na huduma hiyo pia wazawazito watapewa ushauri wa masuala ya lishe maandalizi ya kujifungua sambamba na ugunduzi wa dalili za hatari wakati wa ujauzito,kujifungua na baada ya mtoto kuzaliwa

Katika kuhakikisha mpango unafanikiwa wajawazito wametakiwa kujifunguliwa vituo vya huduma kama vile Zahanati,kituo cha afya ama Hospitalini ikiwa lengo la Kitaifa linatakiwa 80%

Akiwasikilisha takwimu za hali ya wajawazito kujifungulia vituoni Hadija …Mratibu wa …alisema mwaka 2012 waliojifungulia vituoni ni 2112 kati ya 9180 sawa na 23% huku mwaka 2013 waliojifungulia vituoni ni 2779 kati ya 9786 sawa na 28% huku 2014 walikuwa 3389 kati ya 10423 sawa na 32%

Kuhusu uzuiaji wa maambukizi ya VVU Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa motto alisema uwezekano endapo mama hatatumia huduma yoyote ni 5-10% wakati wa ujauzito,10-20% wakati wa uchungu na kujifungua na 5-15% wakati wa kijifungua

Alisema kuwa lengo la Wizara ni kupunguza maambukizi hadi kufikia chini ya 5% akisema kwa Kiteto kati ya watoto 73 waliokuwa wamezaliwa 4 sawa na 5% walikuwa na VVU Ukimwi mwaka 2012,2013 kati ya 103 waliozaliwa 7 walikutwa na VVU Ukimwi huhu mwaka 2014 3 kati ya 91 waliokuwa wamezaliwa walikutwa na VVU

Katika kukabiliana na tatizo hili uongozi wa wilaya kupitia idara ya afya imeendelea kutoa elimu katika maeneo mbalimbali yakiwemo kwenye vituo vya afya sambamba na mafunzo kwa walengwa kupunguza VVU Ukimwi

Katika hatua hiyo wameweza kuwafikia watu maarufu kama vile viongozi wa mila zaidi ya 100 ambayo wanasauti ndani ya jamii kuwapa elimu ili waweze kuelimisha jamii zao waweze kuondokana na tatizo hilo

Wakiwa katika mkutano wa pamoja uliofanyika hivi karibuni kata ya Partimbo baada ya kupata elimu hiyo viongozi hao kwa pamoja waliadhimia kuunga jitihada za idara ya afya Kiteto za kupunguza vifo pamoja na maambukizi ya VVU Ukimwi

Walisema kwa kuwa wanaaminika ndani ya jamii wataenda kuelimisha jamii zao ili waweze kukubaliana na mapendekezo ya wataalamu ambao wamewataka kuhudhuria kliniki sambana na wenzi wao

“Elimu hii ni muhimu sana hakuna anayetaka mke wake ama motto apoteze maisha kwa kutofika kliniki, huko tutakwenda na tutahamasisha wenezu waweze kuona umuhimu wa kufika kwa wataalamu”alisema Lemomo Moringe (laigwanani)
Alisema jamii ya kifugaji inachangamoto kubwa ikiwemo kuwa na wake wengi wakidai suala la kuhudhuria kila mara kiliniki litawapa ukumu kulingana na kazi zao na kuomba Serikali ijenge vituo vya afya karibu nao ili wae na uwezo wa kufika sambamba na upatikanahi wa huduma bora yakiwemo madawa

“Unaweza kwenda Zahanati ya Serikali ukaambiwa kanunua dawa kwenye maduka ya watu binafsi hili linatukatisha tamaa sana na wakati mwingine tunashawishika wake zetu kujifungulia kwa wakunga wa jadi”alise,ma Lemomo

Kwa mujibu wa taarifa toka Serikalini zinaeleza kuwa mpango uliopo kila kijiji kinatakiwa kujenga Zahanati huku kata ikitakiwa kujenga kituo cha afya na Wilaya kuwa na Hospitali ya wilaya ili kupunguza adhaa na usumbufu wa upatikanani wa huduma ya afya

Mwisho

AHSANTE KWA KUENDELEA KUPATA HUDUMA ZETU PIA KUJITANGAZA NASI IWAPO UNAHABARI AMA TANGAZO WASILIANA NASI 0758 222 248/0787 055080
Email . masarade1995@gmail.com ,
ANGALIZO KUMBUKA KILA MMOJA ANA MTAZAMO WAKE HIVYO TUMIA LUGHA NZURI KATIKA KUTOA MAONI YAKO IWAPO UTASHINDWA BASI NI HERI USITOE MAONI SI LAZIMA ILI KUEPUSHA MAKWAZO KWA MWINGINE

Maoni