NDESAMBURO AMUOMBEA KURA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MOSHI MJINI JAFARY MICHAEL


Published in Siasa
Mbunge wa jimbo la Moshi mjini aliyemaliza muda wake ,Philemoni Ndesamburo,akimnadi mgombea Ubunge katika jimbo hilo Jafary Michael (Chadema) katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana katika kata ya Ngangamfumuni.
Baadhi ya wananchi wakiwa kando ya barabara wakifuatilia mkutano huo.
Mgombea Ubunge jimbo la Moshi mjini kupitia Chadema,Jafary Michael akiomba kura wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kata ya Ngangamfumuni mjini Moshi.
Mwenyekiti wa Chadema na mbunge anayemaliza muda wake katika jimbo la Moshi mjini,Philemoni Ndesamburo (katikati) akiwa na mgombea udiwani kata ya Ngangamfumuni,Anthony (kulia ) na mgombea udiwani kata ya Longuo Raymond Mboya. (kushoto).(P.T)
Read more...

DKT FENELLA MUKANGARA AAHIDI KUIJENGA KIMBAMBA MPYA

Published in Siasa
Mgombea ubunge kwa tiketi ya ccm jimbo la kibamba dkt Fenella Mukangara

 wananchi wakimsikiliza Mgombea ubunge kwa tiketi ya ccm jimbo la kibamba dkt Fenella Mukangara.
Na Jimmy Kagaruki,Kibamba
Mgombea ubunge kwa tiketi ya ccm jimbo la kibamba dkt Fenella Mukangara amesema atalifanya jimbo hilo kuwa la kisasa kwa muda wa miaka mitano ijayo.

Dkt fenella ameyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni za ubunge jimbo la kibamba kwenye kata ya saranga.

Akihutubia mamia ya wananchi wa kata hiyo dkt fenella amesema akichaguliwa katika kipindi cha miaka mitano atakabikiana na changamoto za kiuchumi ikiwemo ukosefu wa ajira, miundombinunha barabara, elimu na afya 

Kuhusu chanhamoto ya ajira dkt fenella amesema atahakikisha anazalisha ajira kwa vijana na akina mama kwa kuwaweka kwenye vikundi vya nguvu kazi iki wapate mitaji na iwe rahisi kwao kukopoesheka.

Ameonbeza musema kuwa atahakikisha anaanzisha mtandao wa mawasiliano jimboni humo ikiwemo kituo ca radio ya jamii ( kibamba fm ) ambacho kitakua kiunganishi madhubuti kwa wananchi wa jimbo la kibamba. " najua wananchi wa kibamba mna kiu na shauku ya kuwa na njia ya kuoaza sauti zenu, nawaahidi nitaanzisha radio yenu kibamba fm ambayo itatusaidia kisikuma maendeleo yetu mbele na hata kuzalosha ajira"


Dkt fenella amesisitiza wananchi wa jimbo hilo wasifanye makosa kiwachagua wapinzani bali wachague wagombea wote kutoka ccm ili wapate maendeleo ya kweli.(P.T)
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa Tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, akielekea katika makaburi ya makaburi ya babu na bibi yake mzaa wa baba, eneo la Katoma, wilayani Geita Vijijini huku akiwa ameambatana na ndugu zake ikiwemo baba zake wadogo na mama zake wadogo.
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa Tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, akiwa katika makaburi ya makaburi ya babu na bibi yake mzaa wa baba, eneo la Katoma, wilayani Geita Vijijini akiwatambulisha ndugu zake ikiwemo baba yake mdogo, Michael Magufuli.(P.T)
Read more...

Mbwembwe za rangi katika kampeni za Uchaguzi Mkuu Tanzania 2015

Published in Siasa
Uchaguzi wa Tanzania umekuwa wa kusisimua pengine kuwahi kuonekana katika historia ya Tanzania. Hilo linaonekana wazi kwa jinsi kampeni zinavyoendeshwa kwa mbinu na vivutio vya kila aina. Zuhura Yunus ambaye alikuwa jijini Dar ameshuhudia na kusimulia mbwembwe za rangi zinazopamba kampeni.(P.T) 

UAMINIFU, UADILIFU: CHAGUA JOHN MAGUFULI

Published in Siasa
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wanaCCM na Wananchi wa Jimbo la Mpendae katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM uliofanyika leo katika uwanja wa Binti Amran Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.(P.T) 
Chopa aliyomo Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan ikiwasili kwenye Viwanja vya  Mulowo kuhutubia mkutano wa kampeni jana katika jimbo la Mbozi mkoani Mbeya, jana
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi  baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Mlowo kuhutubia mkutano wa kampeni jana katika Viwanja vya Mlowo jimbo la Mbozi mkoani Mbeya. Pamoja naye ni Mjumbe wa katai ya kampeni za CCM Kitaifa Mwigulu chemba.
Wananchi wakiwa wamefurika Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili kuhutubia mkutano wa kampeni jana katika viwanja vya Mlowo jimbo la Mbozi mkoani Mbeya
Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili kuhutubia mkutano wa kampeni jana katika viwanja vya Mlowo jimbo la Mbozi mkoani Mbeya(P.T)
Read more...

LOWASSA KATIKA MKUTANO WA KIHISTORIA MKOANI MBEYA

Published in Siasa


MDAHALO WA WAGOMBEA URAIS TANZANIA WAFANYIKA

Published in Siasa

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Nghwira (kulia), na Mgombea nafasi hiyo kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Chifu Litayosa Yemba wakijibu maswali mbalimbali katika mdahalo wa wagombea urais ulioandaliwa na Taasisi ya Twaweza Dar es Salaam leo. Hata hivyo wagembea nafasi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.John Magufuli na Edward Lowassa kupitia Chadema hawakuweza kuhudhuria kwa sababu mbalimbali.

 Waongozaji wa mdahalo huo wakiwa kazini. 

 Wadau wakiwa kwenye mdahalo huo.

 Raia wa kigeni na wadau wengine wakifuatilia mdahalo huo.(P.T)
Read more...

MAMA SAMIA AUNGURUMA SUMBAWANGA MJINI

Published in Siasa
 Bando la kumkaribisha Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan,likiwa limeshikwa na wananchi katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine mjini Sumbawanga mkoani Rukwa  jana
 Chopa iliyomsafirisha Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan ikiwasili katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Sumbawanga mkoani Rukwa jana, ambako mgombea huyo alihutubia mkutano mkubwa wa kampeni.
 Chopa iliyomsafirisha Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan ikiwasili katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Sumbawanga mkoani Rukwa jana, ambako mgombea huyo alihutubia mkutano mkubwa wa kampeni.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akipanda jukwaani baada ya kuwasili kwa Chopa, katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Sumbawanga mkoani Rukwa, kuhutubia mkutano wa mkutano  wa kampeni.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia suluhu Hassan akisalimia wananchi baada ya kuwasili kwa Chopa kuhutubia mkutano wa kampeni jana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Sumbawanga.(P.T)
Read more...

DKT SHEIN AMNADI DKT MAGUFULI KISIWANI UNGUJA

Published in Siasa
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein akimnadi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli mbele ya maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.
Dkt Shein emebainisha wazi kwenye mkutano huo wa kampeni kuwa Dkt Magufuli ni mtu sahihi na anatosha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa awamu ya tano atashirikiana nae kwa kila jambo kuhakikisha Tanzania inapiga hatua zaidi kimaendeleo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani Unguja jioni ya leo.PICHA  ZOTE NA MICHUZI JR-KISIWANI UNGUJA.
Sehemu ya umati wa wakazi wa Kisiwani Unguja na vitongoji vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja mjini humo,ambapo Mgombea Urasi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM Dkt John Pombe Magufui aliwahutubia.
Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt Mohamed Shein akimsikiliza kwa makini Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli kabla ya kupanda jukwaani na kuwahutubia maelfu ya wakazi wa kisiwani Unguja kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja,kisiwani humo.(P.T)
Read more...

Williamu lukuvi amembeza mpinzani wake katika jimbo la Ismani

Published in Siasa
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Ismani kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) William Lukuvi 
Na Fredy Mgunda,Ismani
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Ismani kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) William Lukuvi amembeza mgombea mwenzake anayegombea ubunge kwenye jimbo hilo kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema Patrick Olle Sosopi na kusema kuwa Sosopi hata afanye hawezi kuvaa viatu vyake kwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Kauli ya Lukuvi aliitoa juzi wakati akiwahutubia wananchi wa vijiji vya Igingilanyi, Kising’a, Kinywang’anga, Mkungugu, Matembo na Ilambilole vilivyopo tarafa ya Isimani katika Jimo la Ismani alisema kuwa Sosopi hawezi kuvaa viatu vyake kwa kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa maana hana staha ya kuweza kuwashawishi wananchi kuwaletea maendeleo na badala yake anawabeza wagombea wa chama cha mapinduzi CCM pamoja na mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa kusema kuwa kwa kipindi cha miaka 20 ya ubunge wa Lukuvi hakuna maendeleo yoyote yaliyofanywa na chama hicho.
 “Mimi kiatu change navaa namba nane Sosopi anavaa namba moja hivi kweli ataweza kuwa mbunge wa jimbo hili?alihoji huku akishangiliwa sana na wananchi hao,kiukweli niwaambie kama mnataka maendeleo kichagueni CCM ndicho chama pekee kitakachowaletea maendeleo na sio chama kingine.”alisema Lukuvi
Akiwa katika kijiji cha Kinywang’anga Lukuvi aliahidi kuwatafutia wananchi hao madaktari wa kutosha kwenye zahanati zilizopo kwenye jimbo hilo pamoja na dawa za kutosha ili kuendeleza huduma nzuri ya afya kwenye jimbo lake.
Alisma kuwa akatika kuendeleza kuduma nzuri ya afya tayari ameagiza gari ya kubebea wagonjwa(Ambulance) nchini Japani yenye gharama ya Tsh.mil 120 kwa ajili ya zahanati ya kijiji cha Kinywang’anga.
Alisema kuwa kwa sasa  tayari ujenziwa zahanati ya kisinga unaendelea na wanajenga wodi ya watoto,wodi ya wazazi pamoja na nyumba za kuishi watumishi ikiwa maendeleo yote yameletwa chini ya uongozi wa CCM.
Alisema kwa kipindi cha miaka miatano ijayo atahakikisha wananchi wake wanapata maji ya uhakika kutoka Jimbo la Iringa mjini ambayo yanatokana na Mto wa Ruaha.
“ Tayari fedha za kuvuta maji yam to Ruaha kutoka Iringa mjini hadi Ismani tumeshapata,wataalamu tayari wapo na wamesema muda wowote kuanzia sasa zoezi la maji Ismani litaanza”alisema Lukuvi
Aliongeza kuwa uongozi wa serikali ya magufuli hata kabla ya kuamua kugombea Urais tayari alishaweka mpango wa kutengeneza barabara ya Kising’a,Ilambilole,Mikongwi,Ngano hadi Ismani tarafani kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km.35 kwa gharama ya zaidi ya Uro milioni tano ambapo tayari ujenzi huo umeshaanza.
Wakati akihutubia wananchiwa kijiji cha mkungugu alisema kuwa atahakikisha atapandisha kiwango cha elimu kwenye jimbo hilo pamoja na kuweka haki sawa kwa wanawake na wanaume katika kumiliki ardhi.
Hata hivyo alisema kuwa suala la umeme kwenye jimbo hilo kwa baadhi ya maeneo ni la muhimu kwa sababu kuna maeneo yaliyopo ndani ndani hayana umeme hivyo atahakikisha ataleta nguzo kwa haraka ili wananchi hao waweze kuwa umeme.
“ Nitawapigania kuhakikisha umeme unaingia kwenye vijiji vilivyojificha sana ndani ndani na nawaambia lazima nitawaletea nguzo kwa maana mimi mwenyewe jambo la nguzo sitoshindwa.”alisema Lukuvi
Hata hivyo aliwataka wananchi hao kumchagua  mgombea urais wa CCM John Magufuli,mgombea ubunge Williamu Lukuvi pamoja na mgombea udiwani wa kata ya kising’a  Ritta Malagala ili waweze kuwaletea maendeleo ya jimbo hilo na sio mtu mwingine.
Alisema kuwa kwa uongozi wa Magufuli yeye hataki mchezo huu ni wakati wa kazi na sio lelemama na kama kutakuwa na kiongozi ambaye ataonesha amekaa legelege lazima atanyooka kwa maana magufuli hapendi mtu ambae sio mchapa kazi. (P.T)

Maoni