NEC,VYAMA VYA SIASA VYAZIDI KUVUTANA KUHUSU HATMA YA WAPIGA KURA

NEC,VYAMA VYA SIASA VYAZIDI KUVUTANA KUHUSU HATMA YA WAPIGA KURA




 Upo mgongano wa maslahi kati ya Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC)  na vyama vya siasa juu ya mustakabali wa wapiga kura hapo Oktoba 25.
Utata huo unatokana na utekelezaji wa Sheria ya Uchaguzi inayoagiza wananchi kutokuwepo vituoni baada ya kupiga kura.
Kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Uchaguzi, Sura ya 343 inasema, mtu yeyote haruhusiwi kufanya mkutano siku ya uchaguzi au ndani ya majengo ambako upigaji kura unaendelea au sehemu yoyote ndani ya mita 200 ya jengo hilo akiwa amevaa au kuonyesha bango, picha au nembo kwa ajili ya kumpigia debe mgombea kwenye uchaguzi huo.
NEC wameagiza watu wasiwepo kabisa hata kwa umbali huo unaosemwa na sheria na badala yake waende nyumbani ilhali vyama vya siasa vinawataka wafuasi wao wawepo kwa lengo la kusubiri matokeo. Jeshi la Polisi nalo limesema halitokuwa na mjadala na mtu asiyetii sheria kwa shuruti.
Pamoja na mapenzi au mahaba yaliyopo dhidi ya misimamo ya kiitikadi ni vyema kila mwananchi akawa makini na siku hiyo kwa kutambua anachotakiwa kufanya ili kuepusha madhara yoyote yanayoweza kuharibu maisha ya baadaye wakati yule unayempigania akiendelea kusherehekea ushindi alioupata kupitia juhudi zako.
 
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA SIMU NAMBA 0787 055080.0758 222248

Maoni