Tamko la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kukemea vurugu na uvunjifu wa taratibu na sheria


TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Kitalu Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P 2643, DAR ES SALAAM
Simu: +255 22 2135747/8; 2137125; 2135222
Faksi: +255 22 2111281
Barua Pepe: chragg@chragg.go.tz
Tovuti: www.chragg.go.tz

Oktoba 27, 2015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
                                           

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za vurugu zinazotokea katika maeneo mbalimbali nchini wakati huu wa kusubiri kutangazwa rasmi kwa matokeo ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Oktoba 25, 2015.
Aidha, Tume imesikitishwa na hatua ya baadhi ya wanasiasa kuingilia majukumu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ikiwa ni pamoja na kujitangazia matokeo ya uchaguzi kinyume cha taratibu na sheria za uchaguzi.
Tume inapenda kuchukua fursa hii kukemea vitendo hivyo vinavyofanywa na wanasiasa na wafuasi wao ambavyo siyo tu vinaashiria uvunjifu wa sheria, taratibu na kanuni za uchaguzi ambao unaweza kusababisha uvunjifu wa amani na utulivu, haki za binadamu na vitendo vinavyokwenda kinyume na misingi ya utawala bora.
Kwa taarifa tulizonazo vurugu hizo zinazotokea katika maeneo machache ya Tanzania Bara na Zanzibar zimelilazimu Jeshi la Polisi kutumia nguvu, ili kuhakikisha kuwa utulivu na amani ambao tumeushuhudia unaendelea.
Kwa kuwa nchi yetu inaongozwa na utawala wa sheria, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inawataka wadau wote wa uchaguzi waongozwe na sheria za nchi.
Kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi, zinazosimamiwa na NEC na ZEC Tume za Uchaguzi ndizo zenye mamlaka ya kutangaza matokeo ya uchaguzi.
Ili Taifa letu liendelee kuwa na utulivu katika kipindi hiki cha kusubiria kutangazwa rasmi kwa matokeo ya uchaguzi Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora:
1.     Inawataka wadau wote wa uchaguzi wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa, wagombea, watendaji wa mamlaka za uchaguzi, na Serikali kuheshimu sheria za uchaguzi na kila mmoja kutimiza wajibu wake.
2.     Tume (THBUB) inawakumbusha Wagombea wasijitangazie matokeo yao wenyewe ili kuepuka uvunjifu wa sheria na mkanganyiko unaoweza kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.
3.     Aidha, THBUB inawataka wanasiasa na wananchi kwa ujumla wawe watulivu na wasiziingilie kazi za NEC na ZEC.
4.     Inawasihi wanasiasa, wagombea na wananchi kwa ujumla wawe watulivu katika kipindi hiki cha kusubiri matokeo rasmi na wajiepushe na vitendo vinavyoashiria uvunjifu wa amani na haki za binadamu. Kama kuna malalamiko yoyote, sheria na taratibu stahiki zifuatwe
Tume inawataka wananchi watakaobaini uvunjifu wowote wa haki za binadamu, au uvunjifu wa sheria ya uchaguzi, kuzijulisha mamlaka husika zinazosimamia zoezi la uchaguzi. Aidha, wanaweza kutoa taarifa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kupitia ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani (SMS) kwenda Na. 0754 460 259.
Ujumbe lazima uanze na neno 'TAARIFA' au ' RIPOTI' kisha andika taarifa yenyewe. Namba hii inapokea ujumbe mfupi tu. Kwa taarifa zaidi piga Na. +255 22 2135747- 8.
Imetolewa na:
(SIGNED)
Bahame Tom Nyanduga
                                        Makamu Mwenyekiti
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Oktoba 27, 2015
WAANGALIZI WA ULAYA WATOA MAONI KUHUSU UCCHAGUZI MKUU TANZANIA Waangalizi wa Umoja wa Ulaya wamesema uchaguzi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa umeendeshwa vizuri lakini kasoro kadhaa zimesababisha baadhi ya wanasiasa kutilia shaka uhuru wa Tume za Uchaguzi NEC na ZEC. Katika tamko lao la awali mbele ya waandishi wa habari waangalizi hao wamesema kuwa uchaguzi wa mara hii ulikuwa na ushindani mkali huku kukishuhudiwa idadi kubwa ya watu wakijitokeza kupiga kura katika hali ya utulivu na amani. Waangalizi hao wamesema kuwa pamoja na kwamba tume hizo zilijiandaa vyema kufanikisha uchaguzi huo lakini kutokuwepo kwa dhana ya uwazi na kukosekana kwa maelezo muafaka kuhusu daftari la kudumu la wapiga kura kumesababisha kujitokeza kwa hisia mbaya kwa vyama vya siasa juu ya tume hiyo. Waangalizi hao wamesema kuwa mambo hayo kumesababisha pia kwa vyama vya siasa kupoteza imani juu ya mchakato huo wa uchaguzi. Akisoma tamko hilo, Mwangalizi Mkuu wa Umoja huo wa Ulaya, Judith Sargentini, alisema kuwa alikaribisha namna ushindani mkubwa uliojitokeza kwenye uchaguzi wa safari hii, lakini akasisitiza kuwa tamko hilo ni la awali kwa vile bado shughuli za uchaguzi zinaendelea. “Napenda kusisitiza hili kwamba, taarifa hii inatolewa wakati ambapo kazi ya kujumlisha matokeo ingali ikiendelea, hivyo ifahamike kwamba taarifa hii siyo tamko la mwisho kuhusiana na tathmini ya waangalizi wa Umoja wa Ulaya," alisema Sargentini na kuongeza. "Tunavyozungumza waangalizi wetu wanaendelea kufuatilia zoezi la ujumlishaji wa matokeo.” Umoja wa Ulaya ni sehemu ya waangalizi wa kimataifa walioko nchini kwa ajili ya kufuatilia uchaguzi huu ambao pia umeshuhudia baadhi ya vigogo wa kisiasa wakiangushwa kwenye majimbo yao. Waangalizi wengine ni pamoja na Umoja wa Afrika na wale kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC. Aidha waangalizi hao wa Ulaya wamesema wataendelea kusalia nchini hadi hapo Novemba 15, katika kipindi hicho itajihusisha na majukumu kadhaa ikiwamo kukutana na vyama vya siasa, maofisa wa uchaguzi wa asasi za kiraia. Umoja huo umetuma jumla ya waangalizi 141 waliosambazwa katika vituo vyote 625 vya upigaji wa kura. Huu ni ujumbe mkubwa zaidi kuwahi kutumwa na umoja huo kufuatilia uchaguzi wa Tanzania.

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
WAANGALIZI WA ULAYA WATOA MAONI KUHUSU UCCHAGUZI MKUU TANZANIA Waangalizi wa Umoja wa Ulaya wamesema uchaguzi wa Tanzania kwa kiasi kikubwa umeendeshwa vizuri lakini kasoro kadhaa zimesababisha baadhi ya wanasiasa kutilia shaka uhuru wa Tume za Uchaguzi NEC na ZEC. Katika tamko lao la awali mbele ya waandishi wa habari waangalizi hao wamesema kuwa uchaguzi wa mara hii ulikuwa na ushindani mkali huku kukishuhudiwa idadi kubwa ya watu wakijitokeza kupiga kura katika hali ya utulivu na amani. Waangalizi hao wamesema kuwa pamoja na kwamba tume hizo zilijiandaa vyema kufanikisha uchaguzi huo lakini kutokuwepo kwa dhana ya uwazi na kukosekana kwa maelezo muafaka kuhusu daftari la kudumu la wapiga kura kumesababisha kujitokeza kwa hisia mbaya kwa vyama vya siasa juu ya tume hiyo. Waangalizi hao wamesema kuwa mambo hayo kumesababisha pia kwa vyama vya siasa kupoteza imani juu ya mchakato huo wa uchaguzi. Akisoma tamko hilo, Mwangalizi Mkuu wa Umoja huo wa Ulaya, Judith Sargentini, alisema kuwa alikaribisha namna ushindani mkubwa uliojitokeza kwenye uchaguzi wa safari hii, lakini akasisitiza kuwa tamko hilo ni la awali kwa vile bado shughuli za uchaguzi zinaendelea. “Napenda kusisitiza hili kwamba, taarifa hii inatolewa wakati ambapo kazi ya kujumlisha matokeo ingali ikiendelea, hivyo ifahamike kwamba taarifa hii siyo tamko la mwisho kuhusiana na tathmini ya waangalizi wa Umoja wa Ulaya," alisema Sargentini na kuongeza. "Tunavyozungumza waangalizi wetu wanaendelea kufuatilia zoezi la ujumlishaji wa matokeo.” Umoja wa Ulaya ni sehemu ya waangalizi wa kimataifa walioko nchini kwa ajili ya kufuatilia uchaguzi huu ambao pia umeshuhudia baadhi ya vigogo wa kisiasa wakiangushwa kwenye majimbo yao. Waangalizi wengine ni pamoja na Umoja wa Afrika na wale kutoka Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC. Aidha waangalizi hao wa Ulaya wamesema wataendelea kusalia nchini hadi hapo Novemba 15, katika kipindi hicho itajihusisha na majukumu kadhaa ikiwamo kukutana na vyama vya siasa, maofisa wa uchaguzi wa asasi za kiraia. Umoja huo umetuma jumla ya waangalizi 141 waliosambazwa katika vituo vyote 625 vya upigaji wa kura. Huu ni ujumbe mkubwa zaidi kuwahi kutumwa na umoja huo kufuatilia uchaguzi wa Tanzania.

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu

Maoni