HOTUBA YA KWANZA YA MAGUFULI KAMA RAIS HII HAPA


John Pombe Joseph Magufuli (56) ameapishwa mapema leo kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Jaji Othaman Chande Rais John Magufuli alitoa neno la shukrani kwa watanzania na kuwataka washindani wake saba waliokuwa wakichuana katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu kuweka   itikadi za vyama  pembeni na kushirikiana kwa  kufanya kazi kwa maslahi ya Taifa zima.

Amesema kuwa kwa kuwa uchaguzi umekwisha ni vema viongozi hao wakaweka itikadi,maslahi na matakwa yao binasfi kando na kuungana nae kujenga taifa imara.

“Uchaguzi umekwisha na Rais ni mimi John Magufuli sasa ni wakati wa kufanya kazi tu…na nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote na kwa kumtanguliza Mungu mbele,”alisema Rais
Magufuli.

Ameongeza kuwa dhamana waliyopata kutoka kwa watanzania ni kubwa sana na ni jukumu la Serikali ya awamu ya tano kuhakikisha wanatekeleza ahadi zote walizotoa wakati wa kampeni walipokuwa wakiomba ridhaa ya kuliongoza taifa.

Rais Magufuli hakusita kumshukuru Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Wiliam Mkapa ambaye alimteua kuwa waziri wa Ujenzi kwa kipindi chake chote cha miaka 10 wakati huo akiwa na umri wa miaka 35 tu.

Pia alimshukuru Rais Mstafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ambaye naye alimchagua kuwa waziri katika Serikali yake na baadae akiwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpa dhamana ya kupeperusha bendera ya chama hico na kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano ya watu wa Tanzania.

"Magufuli ni nani mpaka achaguliwe na kuaminiwa kuliongoza Taifa hili?," alihoji na kuendelea kusema.. "Nakosa maneno mazuri ya kuongea lakini leo sio sehemu ya kutoa hutuba nipo hapa kushukuru tu"
Mpekuzi blog

Maoni