Mbwa aokolea watoto kifo


                                                               Fisi wa ajabu

Kiteto.Watoto wawili wa familia moja Kijiji cha Kijungu wilayani Kiteto mkoani manyara, wamenusurika kifo kwa kuokolewa na mbwa wao baada ya fisi kutaka kuwaua wakati wakichunga mifugo yao.

Ofisa mtendaji wa Kijiji cha Kijungu Bw.Jula Jula amewataja watoto hao kuwa ni Danniel Gabriel (8) na Olowassa Christopher (12) wa Kijiji cha Kijungu kuwa fisi hao wamekuwa tishio katika maeneo yao

Alisema watoto hao waliona fisi wakiingia ndani ya shimo  kisha kusogelea na ndipo wakatoka na kuanza kuwashambulia na kutaka kuwaingiza ndani ya pango hilo

Wakati fisi wakikamata watoto hao mbwa wao alikuwa akibweka kwa kuona watoto hao wanazamishwa ndani ya shimo ndipo fisi akang’atwa na kushindwa kumwingiza mtoto ndani ya shimo na kuanza kushambuliana na mbwa kisha watoto kutoroka

Kutoroka kwa watoto hao kuliacha kibarua kigumu kwa mbwa wao ambaye muda mfupi aliuawa kisha kuingizwa kwenye shimo lao ambalo hulitumia kama makazi ya kila siku

Ofisa huyo wa Serikali alisema watoto hao wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kilindi kwa matibabu zaidi na kwamba hali zao bado hazijaimarika kutokana na mjeraha waliyopata kwenye mkasa huo

“Watoto hawa wamekimbizwa hospitali ya Kilindi ambako ni karibu tofauti na Kiteto ambako ni mbali kwa lengo la kuokoa maisha yao kutokana na majeraha waliyoyapata”alisema Jula

Kwa upande wa baadhi ya wananchi wakizungumza na MWANANCHI walisema fisi hao wamezoea kuleta madhara katika maeneo hayo na kuiomba Serikali kuingilia kati kuzuia madhara zaidi

Kamanda wa Polisi Christopher Fuime amethibitisha tukio hilo huku idara ya maliasili ikitakiwa kufika katika maeneo hayo kuona namna ya kuwasaidia wananchi hao juu ya wanyama hao

Mwisho



Maoni