Mvua yaleta madhara Kiteto


NA. MOHAMED HAMADA
Mvua kubwa iliyonyesha maeneo mbalimbali  Wilayani Kiteto mkoani Manyara imesababisha madhara makubwa yakiwemo mtoto mmoja kata ya matui eneo la kazi ngumu mwenye umri kati ya miaka 10-12 kupoteza maisha na mwingine kijiji cha Laiseri kuokotwa akiwa hai baada ya kupotea kutokana na mvua hiyo

Katika tukio hilo la mvua pia zaidi ya mbuzi 30 na ngombe 7 zilisombwa na maji kutokana na mvua hiyo na kufa hali iliyosababisha taharuki kubwa kwa wakazi wa Kibaya na Wilaya ya Kiteto kwa ujumla

Kufuatia hali hiyo Wananchi wilayani Kiteto wameitaka Serikali wilayani humo kuona namna ya kuwasaidia juu ya matukio hayo ambayo wengi wao wamepoteza mali zao kutokana na mvua hiyo na kusababisha kukosa makazi na hata mali zao

Mkuu wa Wilaya ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Samuel Nzoka amekiri kunyesha mvua hiyo akisema jitihada za Serikali zinaendelea kuona namna ya kutoa msaada kwa wahanga hao

Mwisho

Maoni