RAIS DR MAGUFULI ASITISHA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI ..,,,



WAKATI Maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani yakiendelea kushika kasi mkoani Singida ambako yalipangwa kufanyika kitaifa mwaka huu Rais Dr John Magufuli ameagiza maadhimisho hayo kusitishwa .

Rais Dr Magufuli ametoa agizo la kusitisha maadhimisho hayo kupitia kwa Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue leo .

Rais Dr Magufuli ameagiza fedha hizo zitimike kununua dawa za kupunguza makali ya ya virusi vya Ukimwi ( ARVs)na vitendanishi vya kupimia Ukimwi .

Taarifa hiyo tayari imefika ofisi ya Mwenyekiti wa tume ya kuthibiti  Ukimwi Tanzania Dr Fatuma Mrisho .

Maoni