RC Manyara aridhishwa na TASAF kusaidia kaya maskini



Mkuu wa mkoa wa manyara Dr Joel Bendera mwenye suti nyeusi wa pili kutoka kushoto akienda kuangalia kaya maskini katika moja wa familia kijiji cha Kiperesa


Mkuu wa mkoa wa Manyara Dr Joel Bendera akimtaka mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Kiperesa ambaye ni kikongwe kuhaa huku yeye akikataa kwa kumheshimu


Mkuu wa mkoa wa Mkoa wa Manyara Dr.Joel Nkaya Bendera ameridhishwa kuona kaya maskini zinazosaidia na Serikali kupitia mradi wa jamii TASAF na kuagiza elimu zaidi itolewe kwa wananchi

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Kiperesa na Njoro baada ya kutembelea kaya hizo Dr Bendera alisema amekutana na walengwa ambao amethibitisha kuwa fedha zilizotolewa na Serikali zimewafikia huku akisisitiza wataalamu kutoa TASAF kuelimisha jamii zaidi

“Sina shaka na mpango huu wa Serikali ambao awamu hii tumeamua kuzijengea uwezo kaya maskini kwa kuwapa fedha keshi ili waweze kukabiliana na umaskini wa kipato tofauti na awamu zilizopita”

Naagiza TASAF endeleeni kuelimisha wananchi juu ya nani anastahili kupata msaada huu kwani kila mahali kumekuwepo na manuguniko ambayo wakati mwingine yanahitaji ufafanuzi tu kidogo

Aliwaasa walengwa kutumia fedha hizo kujikwamua na umaskini kwa kuanzisha vitu vitakavyo wasaidia na kuwapongeza baadhi ya walengwa wakiwemo Bi.Mwanahamisi Issa, Mwanaidi Ibrahimu na Sophia Ramadhani kwa kuanzisha ufugaji kwa fedha hizo

Wakimweleza Mkuu huyo wa Mkoa walengwa hao walisema fedha hizo zinawasaidia kupunguza makali ya maisha kwa kununua mahitaji yao mbalimbali yakiwemo mahindi sambamba na kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku na mbuzi

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini Philipo Sengela mratibu wa TASAF wilaya  alisema mchakati wa utambuzi wa kaya maskini ulianza Julay hadi Agosti 2014

Kaya 7551 zilitambuliwa ambapo kaya 6140 zilihakikiwa na kuandikishwa, huku kaya 1411 zikidaiwa kutopata msaada huo kutokana na kutokidhi vigezo ambapo zoezi la malipo lilianza Julay 2015 kwa kaya 6125

Kwa mujibu wa taarifa hiyo walengwa 15 majina yao hayajajitokeza kwenye orodha ya malipo huku jitihada zikidaiwa kuendelea kufanyika ili majina hayo yaweze kuonekana kisha kupata haki hiyo ya malipo

Alisema malipo ya awamu mbili yamefanyika Julay/ Agost ambapo jumla ya tsh 218,940,000.00 zililipwa kwa kaya lengwa 5684 ambapo tsh 229,368,000.00 ziliidhinishwa huku kiasi cha tsh 10,428,000,00 zikirejeshwa TASAF makao makuu baada ya walengwa 300 kutojitokeza

Malipo ya mwezi Septemba Oktoba kaya lengwa 6111 kati ya 6125 zililipwa tsh 217,208,000.00 kati ya tsh 217,640,000.00 zilizoidhinishwa tsh 432,000.00 zilirejesjhwa TASAF Taifa baada ya walengwa 14 kutojitokeza

Akizungumza kwa niaba ya walengwa hao Yusuph Madi wa Kijiji cha Kiperesa aliipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuzisaidia kaya hizo akisisitiza mpango huo uwe endelevu sambamba na kuwataka viongozi wa ngazi mbalimbali kumuunga mkono Rais John Pombe Magufuli kusukuma maendeleo mbele


Maoni