Madiwani kata 3 CHADEMA wapingwa mahakamani Kiteto



                                                         RAMANI YA MKOA WA MANYARA

Katika kile kilichoelezwa kuwa ni kukaba mpaka penalt Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Kiteto mkoani Manyara kimedhamiria kuufuta upinzani baada ya viti vitatu vilivyochukuliwa na CHADEMA kati ya 20 kupingwa mahakamani

Awali kata zilizokuwa zimetangazwa na msimamizi wa Uchaguzi Kiteto Bosco Ndunguru kuongozwa na CHADEMA  ni Matui,Makame, na Loolera  huku zingine zilizobaki kushikiliwa na CCM ambapo wamesema wanataka kufuta upinzani kwa kuhakikisha CCM inatawala kila kona

Mmoja wa viongozi wa CCM ngazi ya wilaya akizungumza na MWANGANAMATUKIO alisema haoni nguvu ya upinzani Kiteto akisisitiza kilichopo ni chuki inayosambazwa na watu wachjache kukichukia chama akisema safari hii wanaenda kuwatumikia wananchi ipasavyo

Maoni