Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magessa, akifafanua mikakati ya Serikali kuhusu migogoro ya ardhi Kiteto Manyara, Tanzania.
Lemolo Ole Moringe (mfugaji) akizungumzia mgogoro wa ardhi unavyoathiri Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara Tanzania
Mmoja wa wa wakulima Wilayani Kiteto mkoani manyara Tanzania jina hakutaka litajwe akifafanua sakata ya mgogoro wa ardhi na madhara yake
NA. MOHAMED
HAMAD
MKUU wa
wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara, (DC) Tumaini Magessa, amewahakikishia
wakulima na wafugaji, wanaogombania ardhi wilayani humo,kuwa atawatendea haki ili
kila kundi linufaike na rasilimali ardhi
Akizungumza ofisini kwake, Mkuu huyo wa Wilaya alisema,
Kiteto inakabiliwa na migogoro ya ardhi kila upande, akidai njia atakayotumia kwa
sasa ni kushirikisha makundi ya wakulima na wafugaji katika utatuzi huo
“Mashariki
Kiteto tunamgogoro na Wilaya ya Kilindi,Kaskazini tuna tatizo na Wilaya ya
Simanjiro, Magharibi Kondoa na Chemba pamoja na Wilaya ya Kongwa ya Dodoma
upande wa kusini”
Alisema kila
Wilaya ina utaratibu wake, hivyo wananchi wanaohitaji ardhi hasa Kiteto, wanapaswa
kufuata taratibu na sio kuvamia kama ilivyo awali kuwa kila mtu alijitwalia
ardhi kinyume na utaratibu
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti baadhi ya wakulima wilayani hapa walidai kuwa moja ya
matatizo waliyonayo ni pamoja na baadhi ya viongozi wa Sererikali kutokuwa
waadilifu na kujihusisha na vitendo vya rushwa katika kushuhulikia migogoro
hiyo
“Tuna tatizo
hapa, migogoro ya ardhi imekuwa vyanzo vya baadhi ya viongozi, na ukitaka
kushuhulikiwa na haki itendeke kwa wakulima na wafugaji ambao wanadai kila eneo
ni hifadhi ujanjaujanja wa kifedha unaofanywa katika kuanzisha hifadhi
zinazoleta migogoro uachwe”
Alisema
haiwezekani kila eneo likawa hifadhi, lazima Serikali itende haki katika hili
la sivyo kutakuwa na mgogoro usio isha kama ilivyo sasa kuwa viongozi wa wilaya
mkoa na Taifa wamefika Kiteto lakini hakuna utatuzi wa wazi,alisema Bakari
Maunganya (mkulima)
Posted by
mwanganamatukio..
Maoni
Chapisha Maoni