Madiwani Kiteto wataka shule ziboreshwe



 Makamu wa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya, Yahaya Masumbuko akitoa taarifa kikao cha madiwani..
Diwani Hassan Benzi wa kata ya Dosidosi akiwasilisha taarifa ya kamati..
Diwani viti maalumu Rael akiwasilisha taarifa..

Madiwani Kiteto wakifuatilia kikao...



Na, MOHAMED HAMAD
MADIWANI wa halmashauri ya wilayani Kiteto mkoani manyara, wameitaka Serikali kuboresha huduma ya elimu kwa kuongeza samani na thamani shule, ili wanafunzi waweze kupata haki ya kupata elimu kwa kiwango stahili

Wakizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani, baadhi ya madiwani hao  walisema, maeneo mengi wanafunzi  wanalazimika kusomea chini ya miti na kukaa chini kwa kukosa vyumba vya madarasa na madawati

Elia Dengea (CCM), Diwani wa Kata ya Dongo alisema, mazingira ya wanafunzi kupata na kutolea elimu ni duni katika kata yake, akisema kwa sasa hakuna sababu ya kumlaumu mwalimu na hata mwanafunzi kwa kufeli kutokana na changamoto hizo

“Huwezi kutegemea mwalimu kufanya vizuri shuleni wakati anakutana na watoto wanaokaa chini, tena wengine chini ya miti kutokana na kukosa madawati na hata vitabu, kwa hili Serikali inatakiwa kuwa macho katika kulishughulikia mapema kabla ya kujitokeza madhara”

Diwani wa kata ya Dosidosi, Hassan Benzi (CCM), Kassimu Msonde (CCM) wa Kibaya na Kidawa Othman Chadema wa Matui, waliitaka Serikali kuhakikisha kuwa inatimiza wajibu wake wa kutoa huduma hiyo kwa jamii

“Serikali inatakiwa kuhakikisha ujenzi wa miundombinu ya shule inakuwepo , ili kuepuka kila kiongozi kujiamulia kufanya atakavyo kwa kutaka kuepuukana na lawama kama miongoni mwetu wanavyojenga madarasa bila vipimo sahihi, ambayo yanaweza kuleta madhara” alisema Dengea

Akichangia hoja hiyo, Emmanuel Mwagala, Afisa elimu msingi alikiri kuwepo kwa baadhi ya wanafunzi kusomea chini ya miti, na wakiwa wamekaa chini na kuwataka madiwani kuhamasisha jamii kuchangia elimu kwa lengo la kuiboresha

“Ukaguzi tuliofanya hivi karibuni, tumebaini kuwepo kwa baadhi ya madarasa, yaliyojengwa chini ya kiwango tena syiyo na vipimo sahihi, naomba waheshimiwa madiwani kabla ya kufanya hivyo katika maeneo yenu shirikisheni wataalamu”alisema Mwagala

Mwaka jana tuliandikisha watoto 36 elfu, mwaka huu tumeongeza uandikishaji na kufikia 46 elfu, watoto wengi nakiri kusoma chini ya miti na hata kukaa chini, ila sasa madiwani himizeni wananchi kuchangia elimu kwa kukamilisha madarasa alisema Mwagala

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halamshari ya Wilaya, Tamimu Kambona, aliwahakikishia madiwani hao kuwa wakijenga vyumba vya madarasa hadi kufikia lenta kwa kushirikisha wataalamu, serikali itamalizia kama njia ya kushirikishana katika maendeleo

Mwaisho



Na, MOHAMED HAMAD
MADIWANI wa halmashauri ya wilayani Kiteto mkoani manyara, wameitaka Serikali kuboresha huduma ya elimu kwa kuongeza samani na thamani shule, ili wanafunzi waweze kupata haki ya kupata elimu kwa kiwango stahili

Wakizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani, baadhi ya madiwani hao  walisema, maeneo mengi wanafunzi  wanalazimika kusomea chini ya miti na kukaa chini kwa kukosa vyumba vya madarasa na madawati

Elia Dengea (CCM), Diwani wa Kata ya Dongo alisema, mazingira ya wanafunzi kupata na kutolea elimu ni duni katika kata yake, akisema kwa sasa hakuna sababu ya kumlaumu mwalimu na hata mwanafunzi kwa kufeli kutokana na changamoto hizo

“Huwezi kutegemea mwalimu kufanya vizuri shuleni wakati anakutana na watoto wanaokaa chini, tena wengine chini ya miti kutokana na kukosa madawati na hata vitabu, kwa hili Serikali inatakiwa kuwa macho katika kulishughulikia mapema kabla ya kujitokeza madhara”

Diwani wa kata ya Dosidosi, Hassan Benzi (CCM), Kassimu Msonde (CCM) wa Kibaya na Kidawa Othman Chadema wa Matui, waliitaka Serikali kuhakikisha kuwa inatimiza wajibu wake wa kutoa huduma hiyo kwa jamii

“Serikali inatakiwa kuhakikisha ujenzi wa miundombinu ya shule inakuwepo , ili kuepuka kila kiongozi kujiamulia kufanya atakavyo kwa kutaka kuepuukana na lawama kama miongoni mwetu wanavyojenga madarasa bila vipimo sahihi, ambayo yanaweza kuleta madhara” alisema Dengea

Akichangia hoja hiyo, Emmanuel Mwagala, Afisa elimu msingi alikiri kuwepo kwa baadhi ya wanafunzi kusomea chini ya miti, na wakiwa wamekaa chini na kuwataka madiwani kuhamasisha jamii kuchangia elimu kwa lengo la kuiboresha

“Ukaguzi tuliofanya hivi karibuni, tumebaini kuwepo kwa baadhi ya madarasa, yaliyojengwa chini ya kiwango tena syiyo na vipimo sahihi, naomba waheshimiwa madiwani kabla ya kufanya hivyo katika maeneo yenu shirikisheni wataalamu”alisema Mwagala

Mwaka jana tuliandikisha watoto 36 elfu, mwaka huu tumeongeza uandikishaji na kufikia 46 elfu, watoto wengi nakiri kusoma chini ya miti na hata kukaa chini, ila sasa madiwani himizeni wananchi kuchangia elimu kwa kukamilisha madarasa alisema Mwagala

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halamshari ya Wilaya, Tamimu Kambona, aliwahakikishia madiwani hao kuwa wakijenga vyumba vya madarasa hadi kufikia lenta kwa kushirikisha wataalamu, serikali itamalizia kama njia ya kushirikishana katika maendeleo

Mwaisho

Maoni