Mdiwani Kiteto, Serikali boresheni huduma ya elimu


Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Lairumbe Mollel, akisoma dua kikao cha baraza la madiwani Kiteto..
 Diwani wa kata ya Bwawani, Salmu Ng'ungu, akiwasilisha taarifa ya kata yake..
Eliya Dengea, Diwani kata ya Dongo, akiwasilisha taarifa kikao cha madiwani..
Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Lairumbe Mollel kushoto na Mkurugenzi Tamimu Kambona, wakifuatilia mjadala wa kikao cha madiwani..
Wakuu wa Idara wakifuatilia kikao cha madiwani Kiteto..

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Lairumbe Mollel akifafanua jambo..
Katibu wa kikao cha Baraza la madiwani CC. Kituru Othmani akifuatilia kikao
Diwani wa kata ya Dosidosi, Benzi Hassan akiwasilisha taarifa ya kamati ya kamati ya elimu afya na maji..
 Paulo Tunyoni diwani wa kata ya Partimbo akiwasilisha taarifa ya mazingira..

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya, Yahaya masumbuko, akiwasilisha taarifa
 Madiwani wakifuatilia kikao..





 NA. MOHAMED HAMAD


MADIWANI wa halmashauri ya wilayani Kiteto mkoani manyara, wameitaka Serikali kuongeza kasi ya kuboresha huduma ya elimu kwa kuongeza samani na thamani shule, ili wanafunzi waweze kupata haki ya elimu kwa kiwango stahili

Wakizungumza kwenye baraza la madiwani, wakati wakitoa taarifa za kata madiwani hao walisema, maeneo mengi wanafunzi  wanalazimika kusomea chini ya miti na kukaa chini kwa kukosa vyumba vya madarasa na madawati

Elia Dengea (CCM), Diwani wa Kata ya Dongo akitoa taarifa yake alisema, mazingira ya kupata na kutolea elimu yakiwa duni, hakuna sababu ya kulaumu mwalimu na hata mwanafunzi kwani hakuna miongoni mwao aliyekamilishiwa miundombinu ya elimu

“Huwezi kutegemea mwalimu kufanya vizuri shuleni wakati anakutana na watoto waliokaa chini, tena wengine chini ya miti kutokana na kukosa madawati na hata vitabu, kwa hili Serikali inatakiwa kuwa macho katika kulishughulikia”

 
 

 
 

Maoni