3 Jela kwa kuomba na kupokea rushwa Kiteto

Mkuu wa wilaya ya Kiteto, TUMAINI MAGESSA akisisitiza wananchi kuachana na vitendo vya rushwa

3 Jela kwa kuomba na kupokea rushwa Kiteto



Na, MWANDISHI WETU
MAHAKAMA ya hakimu mkazi wilayani Kiteto mkoani Manyara, imewatia hatiani watu watatu wa kada mbalimbali kwa makosa ya kuomba na kupokea rushwa

Waliotiwa hatiani ni aliyekuwa diwani wa kata ya Ndirigishi Chitu Baini (CCM), Katibu wa msitu wa jamii SULEDO, Bakari Hemed na Katibu wa baraza la kata ya Matui Nicodemus Bayo

Akitoa hukumu kwa Diwani Chitu Baini (CCM) aliyeomba na kupokea rushwa ya laki tano, hakimu Elimo Masawe alisema mahakama imejiridhisha kwenda jela miaka mitatu ama faini ya mil moja kwa makosa mawili kuomba na kupokea rushwa

Katika tukio lingine katibu wa msitu wa jamii SULEDO, ulioundwa na kata tatu za Lengatei, Sunya na Dongo, Bakari Hemed amehukumiwa kwenda jela mika mitatu bila faini kwa makosa mawili ya kuomba na kupokea rushwa ya tsh laki saba na nusu

Akisoma shitaka hiyo Hakimu Masawe alisema awali katibu huyo aliwakamata watu watatu watatu kwa madai ya kuvamia eneo la hifadhi ya msitu wa jamii SULEDO na kuwaweka ndani kwa siku tatu mfululizo

Katika mahakama hiyo katibu wa baraza la ardhi kata ya Matui Necodemus Bayo, alitiwa hatiani kwa kuomba na kupokea rushwa ya elfu 40,000 ili aweze kutoa upendeleo kwa mmoja wa wananchi katika baraza hilo

Kwa mujibu wa Mwendesha mashitaka wa kikosi cha kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Isdory Kiyando mahakamani hapo kwa nyakati tofauti alimwomba hakimu kutoa kutoa adhabu kali kwa watuhumiwa hao

Alisema kukamatwa kwa watuhumiwa hao kumetokana na mafanikio ya huduma ya longa nasi ya kupiga simu ya bure (113) ambayo ilifanikisha kukamatwa watuhumiwa hao wakiomba na kupokea rushwa  


mwisho

Maoni