DC Kiteto awaasa wananchi kuchimba vyoo

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Tumaini Magessa..




DC Kiteto awaasa wananchi kuchimba vyoo


Na, MOHAMED HAMAD
MKUU wa wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, mhandisi Tumaini Magessa, amewataka wananchi wilayani humo kuchimba vyoo kwenye makazi yao kuepuka magonjwa ya milipuko

Akizungumza na wananchi wa mji wa Kibaya, mhandisi Magessa alisema, taarifa alizonazo idadi kubwa ya makazi ya wananchi wilayani  humo hayana matundu ya vyoo

Hawezi kuishi ukiwa na afya njema kama makazi yeko hayazingatii usafi, kuwa na vyoo ni kiashiria mojawapo cha kuonyesha mnazingatia afya zenu

Alisema msako mkali utaanza kwa wamiliki wa kaya ambazo hawana matundu ya vyoo katika makazi yao ili kuwashurutisha waweze kuwa nayo kuepuka magonjwa ya mlipuko

Akizungumza na MTANZANIA diwani wa kata ya Lengatei Mainge Lemalali alisema wafugaji wa jamii ya kimaasai Kiteto hawana utamaduni wa kuwa na matundu ya vyoo

Alisema katika maisha yao hujisaidia porini jambo ambalo kitaalamu linaweza kusababisha madhara kama vile homa za matumbo na hata kipindupindu

Kwa upande wa baadhi ya wananchi wakizungumzia agizo hilo walisema, lengo la Serikali ni jema isipokuwa tatizo ni elimu sahihi na kwa wakati ili waweze kufanya maamuzi sahihi

Kemaa Kisiyoo mmoja wa wanajamii ya kifugaji (maasai) Kiteto alisema, wamekuwa na utamaduni siku zote wa kuhamahama na mifugo hivyo sio rahisi kuwa na choo cha kudumu


MWISHO.

Maoni