Jitihada za kampuni ya Namaingo zaanza kuonekana Kilimanjaro

Shamba la mipapai lililopo Same mkoani Kilimanjaro, àmbalo Mkurugenzi wa kampuni ya Namaingo Biubwa Ibrahimu amefika kuona jitihada za vikundi vya  wajasiriamali

Jitihada za vikundi vya wajasiriamali Same zaonekana kwà kuanza uzalishaji kwa wanavikundi chini ya Kampuni ya Namaingo

Na MOHAMED HAMAD

VIKUÑDI vya wajasiriamali KANDA ya kaskazini Arusha na Kilimanjaro  vimeanza kunufaika na kampuni ya Namaingo kwa kuanzisha Miradi ya kuwainua kiuchumi

Biubwa Ibrahimu, ni Mkurugenzi wa kampuni ya Namaingo, yenye makao yake makuu Dar..akiongea na mwanganamatukio alisema lengo la kampuni yake ni kuwajengea wananchi uwezo wakiuchumi

Alisema Namaingo inajukumu la kuwaunganisha wajasiriamali na fursa mbalimbali zikiwemo taasisi za kifedha,wataalamu mbalimbali wa kilimo na mifugo, pamoja na masoko

Katika hahatua hiyo alisema maamuzi ya kuwa maskini au tajiri ni ya mtu mwenyewe baada ya kupatiwa elimu ya ujasiria Mali ambayo hutolewa na kampuni yake

Kwa sasa kampuni ya Namaingo imetandaa nchi nzima ambapo Mkurugenzi huyo anaendelea na ziara kuzunguka nchi nzima kutoa elimu hiyo

Akiwa Manyara Arusha na Kilimanjaro, baadhi ya wanachama walifurahishwa na elimu hiyo wakisema lililobaki ni wajibu wa wao kufanya maamuzi na kumwomba Mkurugenzi huyo kuendeleza jitihada kwa watanzania wengine zaidi ili kwa pamoja waondokane na umaskini wa kipato

Mwisho.



Maoni