Kituo cha habari Kiteto.

Mbwana Juma (kushoto), Mohamed Hamad (katikati) na Abasi Famau kulia..



Kituo cha habari Kiteto.

WILAYA ya Kiteto iliyopo mkoani Manyara, ilizinduliwa mwaka 1974, ikiwa na makabila makuu matao ambayo ni waburunge, wamaasai, wagogo, warangi na wanguu.

Wilaya ina ukubwa wa km za mraba elfu 16,885 yenye idadi ya watu 152,000 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, na kwamba shughuli kuu za uchumi ni kilimo na mifugo.

Harakati za vyombo vya habari ni muhimu kwaajili ya kuharakisha shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii hivyo wajibu wetu ni kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha.

Kuanzishwa kwa kituo cha habari ni wazo lililotokana na wadau na wanahabari mjini Kibaya ambao walihitaji hasa makundi yaliyopo pembezoni (inclusive groups)

Kwa kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, waanzilishi wa chombo hiki ni Abasi Famau (mdau), Mohamed Hamad (mwandishi) na Mbwana Juma (mwandishi).

Katika jitihada za kupashana habari tumefungua ofisi katika jengo la maendeleo ya jamii Kibaya, (Community center) ambayo wakati wote tunapatikana.

Lengo ni kutoa habari za wananchi kwa ukaribu na kwa wakati kwa kiwango stahili ili waweze kufikia malengo tarajiwa ambayo ni maendeleo ya pamoja.

HUDUMA ZINAZOTOLEWA.
Ni kutolewa habari kwenye vyombo mbalibali kama vile, TV, REDIO, MAGAZETI pamoja na mitandao mengine ya kijamii iliyopo ndani ya nchi ya Tanzania

Wadau wa habari ambao ni mamlaka za Serikali, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, idara mbalimbali za serikali za mitaa, taasisi za umma, taasisi binafsi na taasisi za kidini zinakaribishwa.
Kwa mawasilian zaidi waweza kuwasiliana nasi kwa kupiga, 

Simu Na. 0787 055 080), 0656 816 825 0782 867 576 Au 


Imeandaliwa na
Mohamed Hamad
MRATIBU WA KITUO CHA
HABARI KITETO
MANYARA.




Maoni