GGM watakiwa kuheshimu wananchi..

NAIBU WAZIRI MADINI STANLAUS NYONGO AKIZUNGUMZA NA WAKAZI  WA KIJIJI CHA NYAKABALE.
NAIBU WAZIRI, STANSLAUS NYONGO, AKISISITIZA JAMBO..
NAIBU WAZIRI AKISHIRIKI SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MDOGO..
NAIBU WAZIRI AKIPATA MAELEZO YA WACHIMBAJI WADOGO..
NAIBU WAZIRI  AKIMSIKILIZA PILI MWALUKO, ANAEFANYA KAZI YA UCHIMBAJI WA MADINI..



GGM watakiwa kuheshimu wananchi..

Na, Merina Makasi

NAIBU waziri wa madini, Stanslaus Nyongo, amesema Serikali ya awamu ya tano haiko tayali kuona wananchi wakilalamika na badala yake itahakikisha inaondoa manung’uniko hayo.

Baadhi ya wananchi wamekuwa na tabia ya kushuhudia dhulma ikitendeka katika maeneo yao bila kukemea, na kudai kamwe Serikali ya awamu wa tano haitalifumbia macho.

Akiongea na wananchi wa kijiji cha Nyakabale  Mkoani  Geita walikuwa wakiulalamikia mgodi wa gold mine (GGM) alisema Serikali imesikia kilio hicho na itakifanyia kazi.

“Tukikaa kwenye viyoyozi hatuambiwi ukweli na wamiliki wa migodi lakini tunapo fika katika maeneo husika tunapata ukweli , unakuta mtu kazaliwa hapo kakulia hapo amejenga ana watoto halafu anaondolewa huo ni ukatili”alisema waziri huyo.

Aliwataka watu hao wa mgodi kuwalipa wananchi hao ama waondoke wao na kuwaachia eneo lao waendelee kuchimba madini na sio kuwazuia akisema, madini ni neema sio balaa hivyo yasiwanyanyase wahusika.

Akitoa malalamiko mbele ya Naibu Waziri , Joseph Kihengu (mwananchi) alisema, wanaulaumu uongozi wa serikali iliyomaliza muda wake kwa kubinafsisha mgodi huo kwa watu tofauti bila wao kujua.

Alisema wana imani na serikali ya awamu ya tano, hivyo iwatazame kwa jicho la huruma wananchi wa kijiji cha Nyakabele ili wajue hatima ya maeneo yao ambayo yapo ndani ya bikoni mgodi wa GGM.

Katika hatua nyingine akina mama wanyakabale wakiwakilishwa na Godliva Mgini waliutupia lawama uongozi wa mgodi huo kuwataka kuanzisha kikundi cha Baraka baada ya  kuwaahidi kuwawezesha kuanzisha  mradi wa ufungaji  wa nguruwe 100.

Akina mama hao waliambiwa wasombe mawe pamoja na kukamilisha ujenzi kwa gharama ya shilingi laki nane bila mafanikio jambo ambalo liliwagharimu muda na pesa nyingi.

Makamu wa Rais wa mgodi wa GGM Bw. Saimon Shayo akisema wanatambua majirani za na baadhi ya maneno mengine yanafahamika mengine ni mageni hivyo hekima itatumika.

Aidha alisema kuna baadhi ya watu wa nyakabale vigingi vyao vipo ndani ya mgodi kuna watu wana haki ya umiliki wa ardhi kisheria akidai jitihada zilizopo kuangalia  namna ya kutatua tatizo kwa pamoja.

Mwisho.


Maoni