Waziri aonya watoroshaji madini Geita..

                    Naibu  Waziri Wa Madini  Stanlaus Nyongo akiteta na wafanyakazi.



Waziri aonya watoroshaji madini Geita..

Na Mwandishi wetu
Naibu  Waziri Wa Madini  Stanlaus Nyongo, amekea tabia ya baadhi ya watendaji waliopo katika viwanja vya ndege kukosa  uzalendo na kutakiwa kufanya kazi kwa weledi ili kulinda rasilimali za Taifa.

Akiwa katika ziara mjini Geita kufatia taarifa za mtanzania kukamtwa na kilo 32 za madini aina ya dhahabu ambayo yamesafirishwa kupitia uwanja wa ndege wa Mwanza, alionya na kuwataka watanzania kuwa wazalendo.

Mhe. Nyongo  alisema, utoroshwaji wa madini hayo unaofanyika nchini kinyume cha sheria na haukubaliki na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuthibiti kupitia viwanja vya ndege hasa kiwanja cha Mwanza.

"Tunaangalia namna bora ya kuthibiti utoroshwaji wa Madini.. tukithibiti yatasadia kuinua uchumi wa nchi yeyu kwa kiwango kikubwa, kinachofanyika sasa hakikubaliki..’’ Alisema mhe. Nyongo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robart Gabriel, amemuomba Naibu Waziri wa Madini Mhe. Stanslus Nyongo kuundwa kwa kamati maalumu ya kuchunguza kwa kina  utoroshwaji  wa madini hayo.

Aliekamatwa uwanja wa ndege wa Nairobi atakuwa  alitoka Mkoa wa Geita ambao una dhahabu na uwepo wa madini hayo unatokana na uwepo wa miamba mikubwa iliyobeba dhahabu.

Aidha alisema uwepo wa mianya ya  utoroshaji wa madini una sababisha kuikosesha mapato stahiki serikali kutokana na shughuli za usagaji na uoshaji (uchenjuaji) ambazo zimekuwa zikifanyika pasipo uwepo wa sheria.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amemuomba Naibu Waziri wa Madini kuwa, Serikali iangalia ofisi ya madini Geita kwa ukaribu  pamoja na kuiboresha na kuipatia vitendea kazi vya kutosha.


Mwisho.

Maoni