Waziri ataka wananchi walipwe fidia ya mil 202

Mmoja wa wamiliki wa mgodi wa Nyarugusu, akipokea maagizo kutoka kwa Naibu Waziri wa Madini
                        Diwani wa kata ya Nyarugusu, akimpa maelezo Naibu waziri
                          Wananchi wakifungua njia waliyokuwa wameifunga awali..
                Naibu waziri akiangalia mambwawa yaliyoleta madhara kwa wananchi




Waziri ataka wananchi walipwe fidia ya mil 202

Na, Mwandishi wetu
Naibu Waziri wa madini, Stanslaus Nyongo, amewataka wamiliki wa mgodi wa Nyarugusu Mine Company, kulipa fidia ya shilingi million 202, wanazodaiwa na wakazi 123 wa kijiji cha Nyarugusu.

Serikali kupitia wizara ya madini wanayo dhamana, kutoa vibali ama kuwanyang’anya wamiliki leseni ya uchimbaji wanaokaidi na kukiuka sheria na taratibu za nchi.

Katika eneo hilo wawekezaji hao ambao ni wazungu, wanaofanya shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu, wanadaiwa shilingi mil 202 kama fidia ya wananchi 123 baada ya kupata madhara kufuatia kazi hiyo ya uchimbaji wa madini.

Naibu waziri  huyo alitoa agizo hilo baada ya wakazi hao kufunga njia ya kuingia Mgodini, kufuatia madai hayo ambayo wamekuwa wakiyadai kwa muda mrefu bila mafanikio.

Awali wakiwasilisha malalamiko yao baada ya wananchi hao kuzuia njia, kiongozi wa wahanga hao, Shardiraki Mashaka, alisema miezi 4 iliyopita walikosa chakula baada mashamba yao kuingiliwa na maji yenye sumu na kuharibu mazao hali iliyofanya wakose chakula na kuwasababisha njaa.

‘’Kuzuia njia ya kuingia mgodini mmefanya  sawa kwa sababu mnadai haki yenu, nilimtafuta sana huyu mzungu toka jana lakini nina taarifa kuwa polisi wamemakamata tayari’’ alisema Waziri Nyongo

Naye Pili Ramadhani, (mhanga) anasema walishirikiana na serikali kufanya tathimini ya uharibifu uliotokea kwenye mashamba yao na baadae wakaambiwa wafungue akaunti benki kwa ajili malipo yao lakini cha kushangaza  hawakupewa

Alisema mmiliki wa mgodi aliwajibu kuwa katika madai yao wamefanya udanganyifu kuongeza maeneo na kuingiza watu ambao hawastaili kulipwa jambo ambalo sio kweli.

‘’Mhe naibu waziri tumefikia aamuzi wa kuifunga njia ya kuingilia mgodini baada ya kuambiwa tutalipwa fidia lakini mpaka sasa umefika hapa hakuna lililofanyika na uongozi wa mgodi zaidi ya kutuambia tufungue akaunti kwa ajili ya malipo’’ alisema mwananchi huyo.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Nyarugusu alisema tangu November mwaka jana mashamba yao yalingiliwa na matope yenye sumu na serikali ikafanya jitihada kuzungumza na uongozi wa mgodi wa TFC ili walipe fidia.

 Alisema tatizo ilililotokea baada ya wamiliki wa mgodi kuleta barua kuwa hawawezi kutoa fidia mpaka wajiridhishe kutokana na vipengele vyao hapo ndio lililipokuja tatizo.

Akizungumza na mmoja wa mmiliki wa mgodi huo ambae hakutaja jila lake, alisema Naibu Waziri amewataka kwa kushilikiana na mkuu wa wilaya ya Geita kumaliza tatizo ilo ndani ya wiki moja kulipa madai yao tofauti na hivyo Wizara watachukua  hatua za kinidhamu dhidi ya mgodi Uuho wa Nyarugusu.

Mwisho.

Maoni