DC Simanjiro apongeza makundi maalumu kupewa vitambulisho vya kutibiwa

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mheshimiwa Zephania Chaula amewapongeza walemavu 24 na wazee 305 wa Mji mdogo wa Mirerani, kwa kupatiwa vitambulisho vya kuingia ndani ya ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite na vitambulisho vya kutibiwa bila malipo pindi wakiugua.

Ameyasema hayo wakati akiongea na uongozi wa vijana wa CCM chini ya MKT wao Moses Komba hii leo

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Manyara, Mosses Komba katika kikao hicho aliwahakikishia vijana, walemavu na wanawake wa mkoa huo, kupatiwa asilimia 10 za mapato ya ndani kwa halmashauri zote saba za wilaya zilizopo mkoani humo.

Maoni