Kiteto wapata kituo cha afya bora zaidi nchini

Serikali imeboresha kituo cha Afya Sunya, Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, kwa kuongeza majengo matano.

Lengo la kuongeza  majengo hayo ni kupunguza adha na usumbufu kwa wananchi ya kupata huduma ya Afya mbali

Zaidi ya mil 400 zinatumika kuboeresha kituo hicho, kujenga majengo hayo kwa wakati mmoja, kuwaondolea adha wananchi hao

Awali wananchi hawa wanalazimika kwenda Wilaya ya kilindi mkoani Tanga kusaka huduma ya upasuaji na kuongezewa  Damu hali iliyo wapa usumbufu mkubwa

Akizungumza mbele ya mkuu wa Wilaya Omari Puputo (mwananchi) kuwa kituo hicho kikikamilika kitawasaidia wananchi na wataindika na adha kubwa

Kwa mujibu wa uongozi wa wikaya zaidi ya wananchi elfu 30 kutoka nje na ndani ya kata ya Sunya  watapata huduma ya afya

Akizungumza na wananchi hao, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Tumaini Magesa, aliwataka watambue kuwa wamepata kituo bora ambacho hakuna mfano hapa nchini

Aliwataka wananchi hao kuwa na uchungu na kituo hicho kabla ya MTU mwingine hajajitokeza kuwasaidia

Kwa upande wake Dr Mwanaidi,  wa hospitali ya Wilaya ya Kiteto alieleza kuwa kituo hicho kina vyumba maalumu vya kujifingulia, ambavyo hakuna mfano wake hapa nchini

"Hapa kuna vyumba maalum vya kujifulia akinamama, ambavyo huwezi pata kokote nchini, hivyo nawataka wananchi kujivunia kituo hiki na kukilinda"

Mwisho.

Maoni