RC MANYARA, UKUTA WA MERERANI TAYARI

*MAELEZO  YA MKUU WA MKOA WA  MANYARA MHE.  ALEXANDAR MNYETI  KUHUSU KUKAMILIKA  KWA MAANDALIZI  YA  UZINDUZI  WA  UKUTA KUZUNGUKA MIGODI YA TANZANITE  MERERANI, MKOANI  MANYARA .*

Maandalizi ya  uzinduzi wa ukuta kuzunguka migodi ya Tanzanite hapa Mirerani yamekamilika kwa asilimia mia moja.

Niwasihi  wananchi wa Mkoa ya Manyara na Mikoa ya Jirani kujitokeza kwa wingi kesho tarehe 6 Aprili 2018 katika uzinduzi wa ukuta utakaofanyika hapa  Mirerani.

Ujenzi wa ukuta huu unatokana na Dhamira ya dhati ya Rais Wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli.

Jukumu la Kulinda ukuta huu ni la wananchi wote kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na  usalama.

Watanzania  wote wamefurahia  ujenzi wa ukuta huu Kwa kuwa unalenga  kulinda rasilimali zetu.

Wananchi wote wa Mkoa wa Manyara  wanaunga  juhudi za Rais wetu  Dkt. John Pombe Magufuli katika Kulinda rasilimali za Taifa yakiwemo madini.

Ushirikiano kati ya  Jeshi letu la  Wananchi  Tanzania  (JWTZ) na wananchi ni mzuri  kwa kipindi chote cha ujenzi wa ukuta hadi sasa.

Ukuta  huu una urefu wa kilometa  24.5 na unazunguka   eneo lote la migodi ya Tanzanite.

IMEANDALIWA  NA  KITENGO CHA HABARI HALMASHAURI YA MJI WA BABATI

Maoni