SAME YATAKA UWEKEZAJI VIWANDA VYA GYPSUM.
đź’ Ukaguzi wa barabara na maeneo ya uchimbaji madini ya Gypsum Eneo la Chankoko, kata ya Makanya, Same.
đź’ Ni ziara ya Kamati ya ulinzi Same, Ofisi ya madini Mkoa na wataalamu wa Halmashauri.
đź’ Wakutana na wachimbaji na wasafirishaji wa madini hayo
đź’ Barabara ni changamoto kubwa.
đź’ Waonyesha uzalendo, wakubaliana kuchangia kuziba makorongo wakati tunasubiri maombi serikalini. Serikali yaahidi kushughulikia haraka.
đź’ Wako tayari kulipa kodi zote za kisheria. Waomba kikao na DED.
đź’ Wakumbushwa kusawazisha udogo baada ya kuchimba na kupanda miti, pia kuwepo vyoo. eneo la machimbo.
đź’ DC asisitiza kuanzisha viwanda vidogo vya Gypsum na kuchakata hatua ya kwanza
đź’ Zaidi ya leseni 100 zafanya kazi. Eneo latoa ajira nyingi kwa vijana kwani uchimbaji watumia mikono. Ni wachimbaji wadogo. Zaidi ya vitalu 400 havijaendelezwa.
đź’ Wilaya yatenga hekari 4000 za uwekezaji Makanya. Wakaribisha uwekezaji wa viwanda.
đź’ " Pamoja na kutafuta wawekezaji wa nje, kipaumbele chetu ni Watanzania wenyewe njooni muwekeze." Alisema DC.
đź’ Awapongeza wanawake wanaochimba gypsum.
Maoni
Chapisha Maoni