Maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari MANYARA 2018


Mwenyekiti wa MAMEC, Yusuph Dai, akimkaribisha mgeni rasmi, ambaye alikuwa mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akisema siri ya mafanikio ni 
ushirikiano na mshikamano
Nico Mwaibale (mwandishi) akisoa somo kwa wadau wa habari mkoani Manyara siku ya uhuru wa vyombo vya habari mjini Bababti.



NA MOHAMED HAMAD
Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Manyara, ni miongoni mwa walioungana na vyama vingine kuadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini.

Siku hii pamoja na mambo mengine ilikuwa na lengo la kutafakari utendaji kazi wa vyobo hivyo kama moja ya wajibu wao katika kuwatumikia wananchi.

Wakiwa na wadau wa habari mkoani Manyara kwa pamoja waliweza kufanya tafakuri ya namna vyombo vya habari vilivyoweza kuchangia maendeleo ya wananchi na mkoa wa Manyara kwa ujumla.

Mwenyekiti wa Chama hicho, Yusuph Dai, akimkaribisha mgeni rasmi, ambaye alikuwa mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alisema siri ya mafanikio ni ushirikiano na mshikamano

“Mhe Mgeni rasmi, nafasi ya uenyekiti niliyopata kwa kipindi hiki kifupi kuongoza hawa wenzangu siri yake ni ushirikiano, hivyo hatuna budi kuhubiri ushirikiano na mshikamano hasa katika kipindi hiki kwa kuwatumikia wananchi.

“Mara nyingi huwa nasema umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu..mkoa wetu wa Manyara usingeweza kufikia hapa ulipo bila vyombo vya habari, hivyo kama chama tunaomba tuungane pamoja ili tuweze kufikia sehemu tarajiwa”

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akizungumza na wadau hao, alifananisha chombo cha habari kama maji, kuwa hakikwepeki lazima kitumike hata kama hutaki.

“Ndugu zangu waandishi wa habari wa mkoa wa manyara, nitumie fursa hii kuwashukuru sana sana..kwa kazi zenu nzuri mnazozifanya, kama kiongozi wa Serikali natambua mchango wenu.

Huwezi kufika popote kama hutotumia chombo vya habari..Manyara tutaendelea kuvitumia vyombo vya habari ili tuweze kufikia malengo tarajiwa ambayo ni maendeleo”.

Katika hatua hiyo aliwataka waandishi wa habari kuwa na subra katika kazi zao na kuacha tabia za kulazimisha jambo hata kama wanahaki ya kupata habari wasidai na kuwakera wengine

Akiwasilisha mada mbili kwa pamoja ikiwemo  usalama wa wanahabari, Nico Mwaibale (mwandishi) alisema adui wa mwanahabari ni wanahabari wenyewe.

Amewata waandishi wa habari kufanya kazi kwa kufuata misingi na taratibu za sheria za nchi lengo likiwa ni kuihudumia jamii kama sheria isemavyo na kuacha kufanya kazi kwa mihemko.

Mwisho

Maoni