POKEA ZAWADI KWA KUOKOA MAISHA YA MAMA

Hongera zake muuguzi wa mwaka dada yetu Albina kwa kuokoa mtoto na mama kwenye zahanati ya Merr Kata ya Qameyu Wilayani Babati, baada ya kujifungua mama alitokwa na damu nyingi ambapo aliwapakia kwenye bodaboda wakiwa wanne na dereva na kuwafikisha hospitali ya mji wa Babati Mrara, hadi sasa ni wazima wa afya, kutokana na hali hiyo amepewa zawadi ya mabati 10 na wauguzi wenzake na pia mgeni rasmi, mheshimiwa Martha Umbullah akampa zawadi ya shilingi laki moja ya kununua saruji.

Maoni